BINTI NGUVA
Ni hadithi ya kutisha inayohusu safari ya binti kwa jina la Alice katika kupigani maisha ya mpenzi wake Kelvin dhidi ya v majini na viumbe vya kutisha ,katika safari hiyo ianakutana na mambo mengi ya ajavu ikiwa kutenganishwa na familia yake
na kuishi katika dunia ambayo siyo yake
….usikose kufuatilia kisa hiki
UTANGULIZI
Katikati ya bahari moja iliyojulikana kwa jina la BAHARI YA HOPE iliyokuwa karibu na kijiji kimoja kilichojulikana kama KIJIJI CHA KASONGO , palikuwepo siri kubwa iliyokuwa imefichwa, siri ya ulimwengu wa majini, ambao binadamu walikuwa hawawezi kuufikia. Katika ulimwengu huo wa ajabu , alikuwapo , binti mrembo ambaye hakuwa binadamu wa kawaida alikuwa ni samaki mtu ambao wengi hupenda kuwaita NGUVA .jina lake aliitwa Alice Urembo wake haukufananishwa na kitu chochote katika dunia hii, na macho
yake yalikuwa mazuri mithili ya nyota
zing’aazo angani wakati wa usiku. Lakini licha ya uzuri wake, Alice alikuwa na kiu moja – kiu ya kupenda na kupendwa kwa dhati, kitu ambacho hakikuweza kupatikana katika ulimwengu wa bahari.
Upande mwingine wa hadithi, kulikuwa na Kelvin, kijana wa kawaida mwenye ndoto kubwa lakini maisha yake yalikuwa yamejaa changamoto. Hakuwahi kufikiria kwamba hatima yake ingeunganishwa na kiumbe wa ajabu kutoka baharini.
Lakini je, mapenzi kati ya binadamu na nguvu yanaweza kuvuka vikwazo vya dunia
na bahari? Je, nguvu ya upendo inaweza
kushinda hofu, tamaa, na chuki zinazotoka kwa pande zote mbili?
“Binti Nguvu” ni hadithi ya kusisimua ya mapenzi, usaliti, na ujasiri wa kupigania kinachozidi mipaka ya kawaida. Hii ni hadithi ya ulimwengu wawili tofauti, lakini moyo mmoja. Hii ni hadithi ya Alice na Kelvin.
EPISODE 1
hadithi inaanza ikiwa ni majira ya usiku, katika nyumba moja ambayo ilikuwa sio mbali sana na bahari. Kuna kijana mmoja kwa jina la kelvin alishtuka kutoka usingizini baada ya kuhisi kuna kitu kimeanguka kutoka juu ya bati. Alifungua mlango cha ajabu hakuweza kuona kitu . kijana huyu anajihusisha na uvuvi na hakuna mvuvi ambaye alikuwa akikubalika kumzidi kelvin na kila mtu alikuwa anajivunia sana shughuli yake ya uvuvi kwa sababu ilikuwa inamuingizia sana pesa na alikuwa akiitumia kuwasaidia na kuwatumia wazazi wake waliopo mkoani mwanza na wote walimtegemea yeye sio
hao tu hata ndugu walikuwa
wakimtegemea sana kelvin.
Licha ya yote hayo ,hata mabinti waliamini kama wakipata nafasi kwa kelvin watapata maokoto(pesa ) hivyo kila mtu alijaribu bahati yake lakini wapi kelvin alikuwa akiwakataa na kuwambia “huu sio muda wa kupenda ni muda wa kutafuta hela kipindi nmevubaa mlikuwa mnanikataa lakini kwa sasa ….. siwezi kudate na mtu yoyote ” . Wasichana walimchukia sana na kusema “hili kaka lina linga na vihela vyake ,mara oooooh akipata mwanamke ata mvubaza “.
lakini kama wahenga wasemavyo kelele za
chura hazimzuii tembo kunywa maji” . Basi tuendelee jina la kelvin lilivuma sana katika bahari hiyo iliyojulikana kwa jina la HOPE.
BAHARI YA HOPE ilipewa jina hilo kutokana na jinsi lilivyokuwa linavutia sana na aina ya samaki waliopo baharini ndo maana waliipa HOPE ikiwa na maana matumaini na wengi walitumia maeneo ya kando ya bahari kutuliza mambo mbali mbali ikiwa ni msongo wa mawazo ,na kila kitu na iliaminika kila aliyeenda pale na matatizo yake huisha.
Lakini pia kutokana na umaarufu na uhodari wa kelvin wavuvi wengi
walimchukia sana kwa kuona anafanikiwa
zaidi yao . Lakini kelvin alipambana na hiyo hali na ndio maisha ndugu zangu wasomaji ukitaka kufanikiwa usiogope maneno ya watu kwa sababu mwanadamu amepewa mdomo hivyo huwezi kumzuia kuzungumza wewe mtegemee MUNGU tu, kwa sababu hao wanaokusema vibaya vinywa wamepewa na huyo umuombaye na kumtegemea tuendelee sasa …………….
Basi alitoka njee kutazama nini hicho kimeanguka ???? lakini cha ajabu hakuweza kuona chochote akajisemea tena huku akicheka “hahaha… mawenge aya sijuwi nilikuwa nawaza nini mimi ila
sio mbaya ngoja nifanye fanye hesabu
maana leo nimeuza sana samaki na nilipata hela nyingi ngoja nizihesabu ili kesho niende mjini nikaziweke benki ….
Alianza kuhesabu hela zake alihesabu hela kwa muda mrefu sana na hela zilikuwa nyingi sana . mara rafiki yake kipenzi aliyeitwa Goodluck alimpigia simu
. simu iliita wimbo mmoja ambao uliimbwa na msanii aliyeitwa Goodluck Gozbet wimbo huo unaitwa unanipenda kama huujuwi unaweza ukaudownload uusikilize ni mzuri uliimba ivi kabla hajapokea………..
” na nimeamini nikitazama ,
nyuma ni kweli ulinipenda ,
na sikuwa hivi, ila ni wako wema, ni kweli ulinipenda “
kisha kelvin alipokea simu haraka sana na kusema ” namu Goodluck, habari yako “
“aiseeee salama ndugu yangu za huko” alisema Goodluck kwa sauti ya kujiamini.
“kwangu ni salama kaka ,vipi kaka mbona simu usiku , ndugu yangu kuna shida ?? aliuliza kelvin
“ndiyo mwanangu anaumwa sana na sina hela hapo nipo hospitali nadaiwa kama 50000 hivi sijuwi ata natoa wapi !!!!?
” usijali nakutumia sasa ivi si kwenye namba hiii” aliuliza kelvin
“ndiyo kaka nashukuru sana mungu
akulinde rafiki yangu ” alisema Goodkuck akionyesha shukrani kubwa sana ……
“usijali sisi ni ndugu lazima tushirikiane “. Basi maongezi yao yaliisha na baada ya dakika kadhaaa kwenye simu ya Goodluck muamala uliingia imethibitishwa
……………
Goodluck alishukuru maana mtoto wake alikuwa anaumwa sana.
Basi kelvin alihesabu pesa kisha akasema hizi kesho ntaziweka benki na baada ya hapo nitaendelea na mambo mengine , mara ghafla akahisi kama.kuna kitu tena
nje kimepita kama upepo
vuuuuuuuuuuuuuuuuuh …….
Alisita kidogo lakini alimua kuficha hela
.kisha kutoka nje akamuona mwanamke kavaa gaunl refu jeusi huku gauni lake likiburuzika chini .
Alikuwa akitembea kana kwamba anamtaka kelvin amfuate nyuma na kitu cha ajabu kelvin alimfuata kwa nyuma alizidi kutembea huku akiona tu mgongo wa binti na si sura yake alitembea umbali mrefu sana . lakini alipofika mbele aliangaza kila sehemu hakuweza kuona mtu yoyote yule zaidi zaidi upepo tu ukipiga taratibu sio siri aliogopa sana na kujiuliza kwa sauti ndogo”yule binti
nilikuwa namfuata sio muda hapa kaenda
wapi huyu , na angalia sehemu ilivikuwa kubwa na sio rahisi kwa binadamu kutembea haraka hivi ” lakini aligeuka nyuma kwa mbali aliona nyumba yake ikiwaka moto
ooooooh kichwani mwake lilikuja wazo zito “hela” alichomoka kama mshale
,mbio mbio kukimbilia hela zake alikimbia huku anahema sana yaani kana kwamba anakimbizwa na simba na baada ya muda mfupi alikuta hela nyumba yake yote imeungua duuuuh lilikuwa ni pigo kubwa sana alilia kama mtoto …
“yaaani mimi kupapambana kote ,leo malipo ni haya . nani kachoma numba
yangu? na kwanini kaichoma ? sijawahi
gombana na mtu hata kupigizana nao kelele??. kwanini leo wanilipe hivi ???
lakini alihisi kitu na kusema “hebu ngoja kwa hiyo huyu binti alitumwa anizuge yaani anizubaishe ili nyuma yangu wachome mote sio?? lakini je wangechoma nikiwa ndani si ningekufa mimi ? hivyo sielewi binti kanisaidia au yupo kwenye mpango huo wa kuchoma nyumba yangu. Watu wa karibu walifika na kujaribu kuzima lakini haikusaidia kitu
….
Goodluck kwa upande wa pili anapokea simu lakini alisogea pembeni kidogo ili
mkewe asisikie maongezi ghafla sauti
ilisikika
“tumeshachoma nyumba ya kelvin kama ulivotuagiza bosi na yeye amefia humo humo ndani” daaah kweli kikulacho ki nguoni mwako kumbe Goodluck ndo kafanya hila hizo …….
Goodluck alikata simu na kusema ” hahhaah bora ufe haiwezekani mimi nisome mpaka chuo hafu wewe unizidi hela na ukizingatia umeishia kidato cha nne bora umekufa na mtoto wala haumwi nilitaka kujua kama upo nyumbani ” duuuuuuh muda huo kelvin anajua ana rafiki kumbe ni adui
BINTI NGUVA
EPISODE 2
Basi tunaendelea pale pale tulipoishia baada ya kuona kuwa ashakamilisha lengo lake Goodluck alifurahi na kuamua kurejea kurudi kitandani aendelee kulala . lakini bila kujua alichokifanya kimempa maumivu gani rafiki yake ambaye hajaugundua unafiki wake …
UPANDE WA KELVIN
Alibaki ametahamaki pale hana la kufanya hela zenyewe ndo kapoteza sio hela tu kuanzia simu na kila kitu alikipoteza kwa sasa hana jipya mjini waswahili husema
hana chake kimemlamba mmmh
inasikitisha sana lakini alijisemea moyoni mwake ” ridhiki autoye ni Mungu na aitwaaye ni yeye mwenyewe hivyo sitakiwi kulala mika sana ,maana kama imeandikwa nitapata nitapata tu” huku anajipiga piga kifuani .
Mara ghafla mvua ikaanza kunyesha ohoooooo mbaya hiyo kwa kelvin alijaribu kukata majani ya minazi ajistiri lakini wapi radi zilipida sana ikabidi akimbilie kwa rafiki yake
ambaye hawakuwa na ukaribu sana zaidi ya salamu na ilikuwa ni majira ya usiku sana …
Alipofika kwa huyo jirani yake alimgongea
mlango mara tatu ngo! ngo! ngo! yule jirani aliitika kwa sauti nakuja alipofika pale aliufungua mlango na kumkuta kelvin akiwa kanyeshewa na mvua . Alimsikitikia na kumwambia pole sana ndugu kwa yaliyokukuta lakini jaah ni mwema atakuepuehia
Kelvin alijibu “oooooh nashukuru sana maneno yako yananipa nguvu ya kuendelea sasa ndugu yangu naomba nipate hata kahifadhi hata hapa eneo la jiko japo nijistili na haka kamvua sina kwa kwenda zaidi ya kuja hapa kwako kaka……
“daaah najua rafiki yangu huna hadhi ya kulala jikoni lakini unajua nina chumba
kimoja tu na unajuwa mimi , mke wagu na
kichanga chetu ndo kwanza tunajitafuta tafuta hivyo naomba ujikaze tu kwa leo nipo tayari kesho kukupangia chumba ata kwa mwezi mmoja tu rafiki yangu”
hata usjali sana we nisaidie tu nilale hapa kwa leo tu … alijibu kelvin
Emanuel alimpa kelvin blanketi kisha kumuonyesha jiko ili aweze kulala basi baada ya muda wa nusu saa kelvim alipitiwa na usingizi na ikamjia ndoto yq kumstajabisha kidogo ……..
Alikuwa yupo katika shughuli zake za uvuvi alikuwa ndani ya Bahari ya hope akitumia mtumbwi wake mara ghafla hali ya hewa ikabadilika na upepo ukawa mkali kiasi kwamba alipoteza control na kuingia
ndani ya maji ,alikuwa mtalamu sana wa
kuogelea aliogelea cha ajabu akiwa chini ya maji aliona kama geti hivi ilimpasa apite naye baada ya kupita hivi geti lilijifunga akashangaa ametokea sehemu nyingine ambayo ilikuwa ina fanana sana na ya dunia ya kawaida
“Hapa ni wapi tena mbona kama tumeanza kutishana “
Alipotazama mbele aliona kasiri moja kubwa sana napo zungumzia kasiri nazungumzia jumba moja kubwa sana. Alijiuliza nani anaishi pale lakini alikosa majibu alisogea hadi sehemu palipokuwa na geti alilikuta liko wazi …..
Alipotaka kupiga hatua kuingia ndani sauti ya mwanamke ilisikika “usiiiingie humo
ndani utakufa fanya vyote lakini usiingie
humo ..”
Lakini sauti ya pili “Kijana ingia huku ndo kuna sulurisho na ni njia pekee ya kurudi kwenu
Yule binti alimuasa sana lakini wapi alifungua mlango na kuingia alikutana na joka kubwa sana limetanua mdomo tayari kummeza
Hapo alishtuka kutoka usingizini na kujikuta amelala ufweni ilihali ule muda alilala mule jikoni kugeuka alikuta kundi la watu wengi kwenye nyumba ya Emanuel
“kheee imekuaje tene ,kwanza nimefikaje
hapa icho ndo natakiwa kujua ???? na cha pili nini kinaendelea pale ????.
Alisogea mpaka kwenye umati wa watu huwezi amini alikuta Emanuel mkewe na mtoto wake mtoto wake wote wamechomwa Chomwa visu …..
Alijisemea moyoni mwake “nini kinaendelea mpaka mtu ananinyanyua na kunitoa jikoni na kunilaza ufukweni ina maana nina usingizi kiasi gani???
Watu walikuwa wanaongea ongea maneno mengi sana ambayo kwa kelvin yalikuwa yanamuumiza sana sio siri
maana Emanuel alikuwa rafiki yake na
mtu aliyempa msaada …
Alirudi ufukweni akiwa na huzuni na wasiwasi haukupita muda baada ya kukaa pale ufukweni alikuja binti mmoja mrembo sana ana nywele ndefu macho ya kusinzia, ngozi yake lain na nyeupe sio siri alikuwa ni mrembo si kwenye macho ya kelvi tu ata kwa watu wengine ……
Alimsogelea kelvin na kukaaa karibu yake alikuwa katabasamu
“mambo kelvin vipi hali yako kaka” alisema alice akiwa katabasamu
“si salama si unaona huu msiba hapa ni rafiki yangu kipenzi na jirani yangu ,hata
jana tu na mimi nyumba yangu ilichomwa
moto “alisema kelvin kwa sauti ya masikitiko
“pole sana kanambia mama mmoja juu ya yale yaliyokukuta hakika umepitia mengi kaka lakini naamini utashinda zaidi na zaidi cha msingi jipe moyo. Naumwamini mungu …”
Asante sana dada kwa maneno yako hakika yamenipa faraja kubwa sana samahani sikukuuliza j ata jina na sehemu unayoishi ???? aliuliza kelvin
“oooooh naitwa Alice ni mgeni maeneo
haya hata nikikuelekeza huwezi kupajua ila sio mbali sana na hapa !!!!! alijibu alice
Lakini wakiwa wamekaa pale wanaongea mara ghafla mvua ikaanza kunyesha mmmmmh Alice alipatwa na wasiwasi mwili ulipanda joto akawa anatetemeka sana na jasho zipo zinatirrrika tu . Mkono wake wa kushoto ukaanza kutoa magamba enheeeee….nini kitaendelea
BINTI NGUVA
EPISODE 3
Basi tunaendelea pale pale tulipoishia baada ya Alice kuota magamba ya
samaki. ndipo tunapogundua kuwa yule
binti sio kiumbe wa kawaida . Akawa anamwambia kelvin kwa hasira “yatupasa tuondoke hapa kelvin” muda mwili wake ushaanzq kusisismuka mara ghafa kuna kundi la watu walikuwa wanapita mbio mbio hivyo walikuwa wanawapush na kwakuwa msongamano ulikuwa mkubwa sana ….
Baada ya dakika mbili msongamano uloisha lakini kelvin kuja kuangalia vizuri hakuweza kumuona mtu yoyote yule akasema “kheee ina maana huyu Alice kaenda wapi maaana ni ghafla “. Lakini aliona asijali kuhusu hilo suala maana binti alikutana naye pale pale hivyo hata kama kaondoka yeye haimuhusu ….
Alikimbia mpaka upenuni mwa nyumba
moja hivi iliyokaribu sana na eneo hilo maana mvua ilikuwa kubwa na hakuna kwa kwenda ….
Lakini ukisikia siku ambayo ameyakanyags ni leo unajua kwanini ?? kwa sababu mmoja ya mabinti ambaye aliwahi kuwakataa aliishi pale na kwa bahati mbaya binti alimuona akasema “leo nitakuonesha mpumbavu wewe”
duuuuh akachukua maukoko ya ugali na kuyakwangua vizuri huku akisema hakika leo kelvin kayakanyaga yaani alinikata mimi mbona shape ninayo mwendo upo sura nawachanganya wanaume wote hili
eneo yeye anikatae kweli daaah leo
nitamuonyesha
akatoka na yale makoko akijifanya kama hajaona hivi ikasikika ndani haloooooooooooo
Pwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah usoni mwa kelvin kelvin alijifuta na kusema
“nipo hapa jamani najistiri na mvua hiii”
Binti huyo anaitwa tina alijibu yaani kana kwamba ni bahati mbaya “ooooooh sijuwi aiseee sikukuona mara oooih pole jamani mkaka handsome” lakini moyoni mwake
“kelvin wa kunikataa mm kweli sasa huu msimu akiinuka mshale akiinama mshale yaani mpaka aseme mi na kasoro gani
,maana sijawahi kukataliwa na
mwanaume mimi ndo huwa nawakataa kwa nini yeye???
Kelvin alijifuta na akiwa na furaha kidogo”usijali kuhusu hili ni kawaida tu unadhani ni hali ya kuzingatia sana hapana ni vile tu maisha yanavokuwa leo tunapata kesho tunakosa lakini hatupaswi kuacha kupambana ” maneno hayo yalimumiza sana. Tina akajikuta anamuonea huruma kelvin na haraka akaingis ndani na kuchukua kitenge chake na kumwambia kelvin ajifute maana alikuwa ana maugali ugali
MOYONI MWA TINA ……
huku akimfuta kelvin aliwaza “kelvin pole
kwa unayopitia pia nisamehe ni hasira tu jaman sikujua kama unapitia magumu hivi ” huku machozi yakimtoka kelvin akamuuliza unalilia nini sasa????
Tina alijibu “hapana hamna kitu kisha yeye akaingia ndani “
UPANDE WA ALICE
safari ya Alice baada ya kutoka kwa kelvin ilimchukua mpaka katikati ya bahari na hapo alikuwa nusu mtu nusu samaki (NGUVA) Alikuwa akitembea kama mshale mpake sehemu moja palipokuwapo na geti kisha alipoingia geti lilijifunga na akajikuta ametokea sehemu
nyingine (Sehemu hii inafanana na
sehemu ambayo kelvin aliiota kwenye ile ndoto )
Hapo alice alianza kuembea kwenda kwenye lile kasiri alikuwa ana miguu mizuri sana na muda huo alikuwa kavaa kichupi tu …….Kabla hajaingia dada yake kwa jina la sabrina alimwita
………..Aliceeeeeeeee!!!!¡!!!!!!!!!!!!;;;;;;
alionekana ana hasira sana
“hivi Alice mara ngapi una ambiwa usiende kwa binadamu ??? lakini wewe husikii ona leo kidogo ubadilike kuwa samaki mbele ya wanadamu si wangekuu wewe?? alisema sabrina …
“nisamehe dada nilihisi kelvin anahitaji
msaada wangu ndo mana nilienda ” allijibu Alice
” yaani sijawah ona watu wajinga kama wewe Alice hivi huyo kelvin una msaidia kwa nini kazi kumsaidia saidi ulimsaidia siku ile nymba yake ilikuwa ina waka moto sio hapo hata kwa rafiki yake Emanuel nako ulimsaidia pia ?? vipi umempenda au maana sio kwa shobo hizo ..
Alice alijibu “hapana dada siwezi kumpenda adui hata siku moja namsaidia hakuna mapenzi bhana niamnini “
haya sawa twende ndani ila cha msingi
kuwa makini na wanadamu unaweza kupoteza maisha ……… kisha waliondoka na kwenda ndani ya lile kasiri…
UPANDE WA KELVIN
Baada ya mvua kupungua tu alitoka na kuelekea maeneo ya sokoni ambapo alipofika huko alikuta na mzee ismail moja kati ya wateja wake wakubwa sana na mzee alipomwona alimpa pole kwa yote yaliyomkuta na kelvin alimwambia mzee anatakaa arejee mwanza akafanye mambo mengine lakini mzeee alimwambia hatakiwi kuondoka na kama hana nyumba yule mzee atampa nyumba
akae bure na hataki malipo yoyote yale
………….
Kelvin alifurahi san na kusema “hakika uishi maisha marefu mzee ismaili hakika wewe ni mwema kisha kelvin akapiga magoti mzee akamwinua na kusema wa kuabudiwa ni mungu na sio mimo mimi nimekusaidia wewr mwanangu kwa kuwa ulinisaidia mara nyingi kipindi sina hata mboga nyumbani kwangu …
NDUGU MSOMAJI CHA KUKUSIHI NI KWAMBA WEMA NI AKIBA NA UBAYA NI AKIBA UKIMTENDEA MTU MAMBO MEMA UTALIPWA MEMA UKITENDA MABAYA UTALIPWA MABAYA USISUBIRI JAMBO ULILOTENDWA ULIPWE HAPO HAPO
WEWE SONGA MBELE LAKINI JUA KUWA
UMEWEKA AKIBA NA AKIBA HAIOZI
.,………….. …………………
Lakini kumbe nyuma ya yote kuna binti alikuwa anamfuatilia alimpigia simu Goodluck na kumwambia kuwa kelvin yupo na ismaili Goodluck alimwambia aendelee kumfuatilia ajue wanataka kufanya nini ??? lakini alipomaliza kuja kuwatazama hakuweza kuona mtu walikuwa washaondoka
Alisema “wameenda wapi hawa watu
?????
Inaendelea