PISI YA KIJIJI
EPISODE 7
Sehemu ya saba inaanza muda ule ule ambao OLESTA aliondoka pale kwa mangi alikuja lucy kavalia kisuruali
kina mbana sana kikionyesha maungo
yake na alimtazama mangi na
kumwambia
“sasa baby nina shida mwenzio” “shida gani tena baby???”
“nyumbani sina mchele wala mafuta na sina hela “
“sasa mimi si nipo unawaza nini my love”
Akaanza kumpimia mchele kilo tano na mafuta kidumu kimoja alimpa na mwishowe alimwambia” usiku njoo kwenye muembe nina zawadi kwa ajili yako mpenzi”
Basi akaondoka zake huku
akiyatingisha mauno yake na kumfanya mangi atoe udenda huku akisema “chombo cha mimi ,chombo cha mangi nipewe nini mimo kama sio mtoto mrembo kama huyu “. Basi tunaendelea palepale Olesta alipoingia ndani na kumkuta kelvin aliangusha kila kitu lakini alipogundua baba yake yupo ndani ilibidi atulize jazba zake ..
“Mwanangu huyu kelvin ndo alinisaidia ile siku”
“Asante kelvin kwa msaada wako kwa baba yangu”
“Usijali olesta tupo pamoja sana sisi
binadamu inabidi tusaidie”
Aliendelea “Sawa baba mi ngoja niwaache nawahi nyumbani nikasaidie wazazi kazi”
Baba olesta”hamna shida kijana hebu Olesta msindikize kaka yako utarudi upike “
Basi walitoka nje kelvin na olesta na walionekana kwamba kila mtu anahasira na mwenzie lakini kelvin kuona oleata kageuka na kutaka kurudi ndani alimvuta na kuwafanya
wasogeleane zaidi Olesta akajitoa
mwili na kusema “kelvin sitakiiii” “iam sorry olesta “.
“kelvin m nimesema sitaki”
“haya basi powa baki hapo hapo” aliondoka kelvin kwa hasira hata olesta naye aliingia ndani kwa hasira
……..
OLESTA NDANI KWAKE
“Yaani li mwanaume limenikosea halitaki kuniomba msamaha yaani sijuwi likoje baada ya kuwa mpole anakuja juu yaani kweli atakuwa
hanipendi kabisa alijitupa kitandani
huku akiufinya mto kwa nguvu
KWA KELVIN NAKO
“Yani wanawake wengine bhana yaani wanakosewa tunajishusha hawaelewi bwana eeeh kila mtu apambane na mambo yako alifungua mlango na kuubamiza kwa hasira sana
“Paaaaaaaaaaaaaaaaah!!!!!!!!!!!!!¡!!!!!!!
!!” mpaka funguo ikaanguka …..
Basi siku hiyo ilipita na baada ya siku mbili baadaye barabarani kato ya olesta ilikuwa pita nikupite na kelvin
hilo hata hakujali kwa sababu yeye
alimchukulia olesta kama rafiki muda huo olesta anamchukia kama mwanaume ambaye hawezi kulala bila kutaja jina lake ……
Haya kwa lucy naye alikuwa yupo na marafiki zake mara honi ya gari ikalia pipiiiiiiiiiiiiiii na kioo kikashushhwa na baba mmoja alionekana lucy alifurahi sana na kukimbilia karibu na lile gari na kisha alipofika pale karibu na gari aliupenyeza mdomo wake mpka kwenye shavu la yule mubaba na kumkiss
mwaaaaaaaaaaaaaaaaah mubaba
wangu
nimekumos jamani habari za Dubai jamani??
“habari za huko salama kabisa”
“jamani ulivoenda nilijuwa hutarudi” alianza kudeka
“kwanini nisirudi wakati furaha yangu ipo kwako jamani panda twende nikupeleke sehemu nzuri”
Lucy aliingia kwenye gari na kuondoka na yule mubaba hakujali kuhusu marafiki zake yeye ni bata kwanza mambo mengine yatafuata basi
alimpeleka sehemu moja nzuri sana
akamnunulia chakula na kumfanyia kila kitu ilimradi awe na furaha na mwishowe walichukua chumbani cha bei ghali sana .Na mwishowe mlango ulifungwa na sauti za mabusu zilianza kusikikan ndani mara milio ya mahaba nayo ikiwa na maana tayari lucy katafunwa ……
SIKU ILIYOFUATA
Maeneo ya hospitalini sauti ya viatu vilisikika vikigonga chini ikiashiria kuna jamaa anapiga hatua kwenda ndani kila alipopita watu wote walikuwa
wakigeuka kumtazama yaani sio
wazima tu hata wagonjwa kwa wanawake ndo walikuwa wakipagawa na sauti zilisikika “jamani huyu kaka ni handsome “
“kijiji kizima hakuna handsome kama huyu yaani siwezi ishi bila yeye “
Jamaa alitowa miwani yake na kuachia tabasamu kisha kusonga mbele bado hajaonekana sura je atakuwa ni nani ???
EPISODE 8
Basi mtu yule jamaa alifika mapokezi
ambako huko alikutana na mariam na alimtazama maana aliamini hakuna mwanamke ambaye hatamuona asimzimie akamwambia kwa madaha
” mambo mrembo”
“powa karibu” alionekana hana muda na yeye
“hebu nitazame acha ubize” “tayari vipi kuna nini kwani ” “nionyeshe kwa mganga mkuu “
“huko nyuma ukipita hiyo korido kuna hodi la watoto angalia mbele utaikuta ofisi”
jamaa aliondoka lakini alijiuliza mbona
binti kanichulia wakati anajua kuwa mimi samwel au waweza niita MR HANDSOME mtu mwenye pesa nyingi sana . Aliingia kwa mganga mkuu naye alimpokea na haikupita muda aliitisha kikao na kumtambulisha kwa kusema huyu ni mfanya kazi mpya yena idara
ya upasuaji mpeni sapoti yenu anaitwa Mr Samweli. Alipotajwa jina jinsi anavyopenda sifa alikuwa anaweka tai yake vizuri sana ….
KWA BAHATI NZURI AU MBAYA …mtu
liyeambiwa amuonyeshe mazingirabya hospitali alikuwa ni mariamu. basi
mariam alimzungusha mwishowe
baada ya jamaa kuridhika na kujua baadhi ya maeneo akamwambia
” unaonaje tukapate supu panoja” “mmmmmh hapana kanywe tu”
Unaambiwa Mr Romantic toka aanze kuwaalika wanawake iwe lunch iwe dinner n hakuna aliyewahi wahi kukataa hali iliyomfanya ashtuke sana na kujisemea moyoni mwake
“mmmmmh huyu mwanamke yaani hataki shobo na mimi duuuh haijawah tokea mwanamke kunikataa mimi yaani kapata wapi ujasiri ????
Haikupita hata sekunde kumi alokuja
kelvin hapo hapo hospitali na alikuwa kasimama kwa mbali kumuona binti akiwa anaongea na yule jamaa na akimtazama jamaa alivyobishoo ba wanavyoobgea aiseee wivu ulimshika aliumia kuliko hata kawaida. Aligeuka nyuma tayari kwa kuondoka zake alipiga hatua tatu tu na mariami katika kuongea ongea ile anageuka anamuona kelvin akiwa anaondoka alimuacha Mr Romantic pale pale na kumkimbilia kelvin …
Alifika na kumvuta mkono kisha akasema
“kelvin mbona unaondoka bila
kuniona??”.
“hapana niliona uko na mtu mwingine tena mnacheka”
“kwa hiyo umekasirika ???”
kelvin alimtoa mkono kwa hasira ” ndiyo nimekasirika tena sana ,mtu unachekea na mwanaume huku wengine wanawachungulia madirishanina unataka nifurahi sio”
Ujuwe kelvin hajawahi kumtongoza mariamu lakini wivu anauonyesha hapa inaonyesha dhairi shairi wana mahusiano hali iliyomchanganya
mariamu sana na kumuuliza .”kwani
mimo na wewe ni wapenzi au ni vipi mbona sikuelewi kelvin”
kelvin alijishtukia na alimwambia “am sorry nimevuka mipaka ” kisha akaondoka zake ….
Nakumuacha Mariamu akimsindikiza kwa macho tu lakini hapo ndipo kwa hesabu za haraka za Mr Romantic akagundua kuwa kuna kitu kati ya hawa wawili ……….
KWA MANGI GENGENI
Alikuja cholo gengeni ali maarufu kama MMBEYA wa mtaa yaani yale
matukio yote ya lucy aliyaona kama
anaangalia Tv hivyo ni muda wa kusimulia sasa na alionekana ni mtu wa serious sana kumbe umbeya tu
“Mangi inakuaje”
” flesh karibu cholo” huku akijikoki “we jamaa lucy si unapita naye” “uhakika ile ni pisi yangu soon naoa” “make kwanza nicheke mie” cholo
alipiga kofi moja kwa mikono yake hali
iliyomfanya mangi awe na wasiwasi ” mbona unacheka kuna nini”
“tafuta mwanamke wa kuoa sio lucy” “lucy ndo chaguo la moyo wangu”
“Mangi nielewe mimi jamaa”
“nakuelewa vp hujanielekeza au unamtaka lucy”
“nimtake lucy nimpeleke wapi huyo binti hana maana yoyote binti malaya kila kukicha bwana mpya utapata magonjwa wewe mbona kijiji kuna pisi nyingi sana “
“Ndo maana nilimchagua yeye katika wengi …”
“karaga bhao na ujinga wako” Alisema Cholo na kusepa zake kwa hasira …..
Na mangi alikuwa akijisemea maneno ya kujinadi”Mti wenye matunda lazima
upigwe mawe na lucy simuachi unajua
ni vingapi acha usenge (huku mangi akikunja sura akionyesha kuchukizwa na maneno ya cholo)
Basi baada ya hilo tukio maeneo ya cantini ya hospitali ndipo Mr handsome (samweli)alikuwa anaweka nywele zake vizuri na kuingia cantini kwa bahati mbaya alipokuwa anatembea kwenda kukaa alipamiana na binti mmoja mrembo sana.
Mfanyakazi wa hiyo cantini kazi yake ni kusambaza na kupeleka chakula jina lake ni Isabella. binti mmoja mrembo sana
Alisema “sorry kaka ni bahati mbaya “
Binti kuja kumtazama usoni alidata hapo hapo na kujikuta wakitazamana
EPISODE 9
Inaaendelea pale pale ambapo macho ya mr Romantic yalipokutana na isabella na walikuwa wakitazamana huku isabella akiachia tabasamu licha ya kuwa muhudumu wa cafteria ya hospitali lakini mavazi yake hayakufanya urembo wake ufichike si tabasamu na hata mapozi …. lakini
kwa Mr romantic warembo kumzimia
ni kitu cha kawaida sana na si jambo geni hapa jijini….
Walishtuka na isabella alikuwa wa kwanza kuongea
“oooooh sorry kaka sikukuona”
“usijali najua uko bize na kazi zako , hivyo kuwa na amani dada “
“nashukuru sana pia karibu sana “
“asante sana ” huku akikaaa kwenye kiti na kuagiza supu na chapati …..
Binti alimuhudumia na kwenda kukaa kaunta macho yake yote kwa Samweli anavyokula anavyomeza mpaka rafiki yake kwa jina la Tina alipomshtua
“weee isabella unaangalia nini”
“hapana bhqnaaawaaaa” akizuga zuga “au ushampenda yule kijana “
“hapana bhana si namuangalia tu”
“mmmmmmh shoga yanga acha uongo” huku akimtikisa bega
“,hapaana bhana kwanza niache kidogo”
Baada ya muda Mr romantic au Samwel aliamua kwenda kuosha mikono yale na sanitizer kisha akajifuta na tishu na kipindi anatoka isabella alimkimbiilia na kumwambia
“samahani kaka umesahau chenji
yako”
“oooooooho mambo ni mengi muda mchache but baki nayo mama “
“mmmmh hapana bhana ,chukua “
“baki nayo please nachelewa kuna mahala naenda “
“okay nitajie basi jina lako please” “naitwa samweli wewe je”
“naitwa Isabella “
“nice name sasa mimi naenda ” “okay byeeee”
“byeee”
Lakini Recho hakuchoka kumtazama
Samweli kila anapopiga hatua kwenda mbele yeye alimsindikiza kwa macho tu ….
UPANDE WA GABRIEL
Gabriel alikuwa yuko busy na mishe zake kwq mbali alimuona maximiliani anakatisha sehemu na ni muda sasa hawajaonana alimkimbilia na kumuita “dada ” Mariamu hakuwa na hiyana aligeuka na alippmuona ni yule kijana aliyekutana naye pale sokoni siku nyingi za nyuma alisimama na kumsubiri….
“mambo mrembo nawe ndo
umepotea”
“hapana sio hivo jamani mambo mengi”
“haya unaitwa nani hukunitajia jina lako”
“mmmmmh mbona nilikutajia ” “acha uongo bhana hukunitajia ” “okay naitwa Mariamu “
“naitwa Gabriel”
“Wow jina zuri unaelekea wapi” “mi naelekea zangu nyumbani “
“ooooops basi sawa mi nataka nirudi kazini mara moja “
“unakaa wapi ulisema utaniambia”
“kwa mzee Mwakatobe hapo karibu na kota za mwisho za hospitali”
“tukijakukutembelea ysitufukuze’ “usijali karibu kwa heri Gab ” “okay byeee mamu..”
Mariamu alikuwa anakimbia kuelekea hospitalini huku Gabriel akimsindikiza kwa macho …..
Na kusema “lazima nikupate iwe jua iwe vua ila sidhani uko single lakini kwako nitan’gan’gana” kisha naye akasepa zake
UPANDE WA KELVIN
siku iliyofuata kelvin anachotelea maji kuyapeleka nyumbani lakini kumbe dirishani olesta anamtazama kwa mbali huku kaweka mikono mashavuni “jamani hata nikikununia bado nakupenda tena sanana leo lazima nitakwambia sijuwi utanichukuliaje ni bora ujuwe nini kina usumbua moyo wangu ,nimechoka kuwa sugu wa mapenzi “
Alitoka nje na kujisemea moyoni “leo lazima niseme yaani nataka niwe huru naye siwezi kulifumbia macho hili jambo …….
Alimfuata kelvin mpaka bomba na kuzungumza naye kidogo
“kelvin habari za asubuhi” “flesh vipi”.
“safi kabisa bado umeninunia “
“hilo swali nikuulize wewe alikuwa namjibu kana kwamba hana muda naye baada ya kumaliza kukinga maji akawa kabeba ndoo zake moja kulia moja kushoto ….. lakini sauti ilisikika
“kelvin kuna kitu nataka nikwambie leo”
“sema nakusikiliza ujuwe nawahi nyumbani “
“okay lakini usinifikirie vibaya “
“usijali we semaaaa Olesta “
“kelvin nakupenda sana toka zamani”
kelvin kusikia hivo mwili ulikufa na ganzi na kujikuta anaachia ndooo zile chini na maji kumwagika akili iliganda alimgeukia Olesta ambaye alisema huku machozi yakimtoka.
Alibaki anamtazama tu je nini kitaendelea usikose sehemu ya 10