PENZI LA KIKOMANDO
EPISODE 04
ILIPOISHIA….
Mke wa General Ramos anamfuata mmewe akiwa ameshika barua mkononi na kumwambia mtoto wao atakuwa amefariki
INAENDELEA…..
NDANI YA MSITU
“Wonder nashukuru kwa msaada wako, lakini sikuhitaji tena wewe endelea na safari yako na mimi niende na njia yangu sawa……?” Aliongea James kwa msisitizo sana akiwa anachukua siraha yake iliyokuwa chini na kuanza kuondoka.
“Wewe mwanajeshi kijana mbona ni mgumu sana kuelewa, nimesema mimi naongozana na wewe kuelekea huko unakoenda …” Aliongea wonder akiwa anamfuata james kwa nyuma.
James anajitahidi kumzuia wonder asimfuate lakini wonder anazidi kuwa king’ang’anizi inamfanya James akubali kuongozana na wonder safari moja.
James alitembea umbali mrefu sana, nyuma yake alikuwa wonder akimuongelesha James kwa ucheshi lakini James hakuonekana kuongea njia nzima yeye alikuwa akitazama mbele yake tu .
“ Wewe ni bubu ety, hivi uko kambini kwenu tunafika saa ngapi ?…..” Aliuliza wonder alipoona James yupo kimya kwa mda mrefu .
“ Tukimaliza kupanda ule mlima wa mbele tutakuwa tumefika kambini …._”Aliongea James akiwa anaendelea kukatiza kwenye vichaka vya miba .
“Maajabu sasa hivi umeongea maana mmmh …” Aliongea wonder akiwa anakwepa miba iliyokuwa mbele yake.
“Aaaaaaaaaaaa……” Alilia wonder baada ya mwiba mmoja kuingia ndani ya kiatu lakini James hakugeuka nyuma aliendelea na safari yake.
“Nisubiri basi … “ Aliongea wonder akiwa anakimbia kwa kuchechemea mguu mmoja.
NDANI YA KAMBI
Mke wa General anamkabidhi mmewe barua aliyoandika mtoto wao kabla ya kuondoka huku akiendelea kulia .
General Ramos anachukua haraka barua na kuanza kuisoma
“ Baba , mama samahani sana ila nimefanya maamuzi ya kwenda kupambania kitu nilichokuwa nakitamani tangia nikiwa mdogo , nataka niwe shujaa sasa naombeni baraka zenu …” Yalikuwa ni maandishi yaliyoandikwa ndani ya ile barua.
“Binti yangu atakuwa alienda vitani maana alikuwa anaomba sana nimruhusu ila nilimkatalia, eee Mungu naomba binti yangu awe salama tu ….” Aliongea General kwa woga sana baada ya kumaliza kusoma barua.
General anatoka pale aliposimama kwa kasi sana kuelekea sehemu wanayofanya mazoezi wanajeshi .
“ Andaeni siraha zenu haraka tunaenda kumtafuta mwanangu msituni…” Aliongea General kwa sauti kali akiwaambia wanajeshi wote waliokuwa wakifanya mazoezi.
MSITUNI
“ Huu tukimaliza kupanda huu mlima tunatokea kambini ety afande kijana? …” Wonder alimuuliza James wakiwa ndo wanaanza kupandisha juu ya mlima .
“ Ndio , ila kwanini wewe ni mwanamke mrembo alafa unajiingiza kwenye mambo ya hatari ?” Aliuliza James akiwa anaendelea kutembea
“ Ni kitu ambacho napenda tangia zamani , kupambania watu wengine pamoja na taifa langu ni hivyo tu afande kijana….” Alijibu wonder .
Wakiwa bado wanaendelea kupanda mlima ghafla kundi kubwa la waasi linatokea mbele yao juu ya mlima likiwa na siraha .
“Mrembo Tukimbieeeeeee….” Alimwambia wonder kwa sauti ya juu alipowaona waasi nyuma yao. James haraka sana anamshika wonder mkono na kuanza kukimbia kuelekea nyuma walikotoka
“Ongezini kasi mpaka tuwakute Hawa vikaragosi…” Aliongea Aboku kwa sauti kubwa akiwa anakimbia na wenzake kuelekea wanapoelekea wonder na James.
“James siwezi tena kukimbia nimechoka Mimi….” Aliongea wonder kwa kukosa pumzi akiwa anapunguza kasi yake.
James anamnyanyua kwa haraka na kumuweka begani kisha anaendelea kukimbia nae.
Bila kusimama wala kutazama nyuma wanafika eneo ambalo lilikuwa kimya sana.
“Hatimaye tumefanikiwa kuwakimbia waasi…..” Aliongea wonder akiwa anashuka mgongoni kwa james, james alikaa chini akiwa anapumua kwa nguvu..
Dakika chache mbele wakiwa wamekaa pale chini wakipumzika ghafla waasi wanatokea katika kila upande na kujikuta James na wonder wapo katikati ya Jeshi la Aboku.
“Hahahaha vijana wadogo nyie mlidhani mtaweza kutuingiza mjini sisi ….”aliongea Aboku Kiongozi wa waasi taratibu akiwa anasogea sehemu waliyokaa James na wonder.
Wonder kwa woga anasogea karibubu na James. James anageuza mkono wake nyuma na kushika siraha kubwa aliyoweka nyuma ya mgongo wake.
“Kijana usijaribu kufanya chochote maana unaweza ukauliwa , tena sio peke yako hata huyu binti ataulowa kwa hiyo kuwa mpole tu…”Aliongea Aboku alipomuona James anataka kuchukua siraha.
Taatibu Jamesbanaaiachia siraha na kuunyosha mikono yake miwili juu .
“Niuweni mimi ndo mwenye makosa huyu binti muacheni aende hana hatia …” Aliongea James mikono yake akiwa ameweka juu huku akimtazama wonder.
Aboku anamsukuma wonder pembileni na kumfunga James kamba ngumu .
“ Usinipangie cha kufanya kijana , ila sawa kivile umeomba nitamuachia binti na wewe utabeba adhabu yake, utauliwa mbele ya huyu binti….”Aliongea Aboku kwa hasira akiwa amemkaba James shingoni kwa nguvu..
“Muacheni aende nitawapa Gold key original….” Aliongea wonder anakabwa .
“Ipo wapi hiyo Gold key original au unataka utuchezee kama mwanzo?……”Aliongea Aboku akiwa amemuachia James na kumsogelea wonder.
Wonder anaingiza mkono wake nyuma ya mfuko wa suruhali yake na kutoa Gold key.
“ Hii apa mfungueni James ….” Aliongea wonder akiwa ameshika gold key mkononi .
Abokubkwa haraka sana anaichukua gold key milkononi kwa wonder na kuanza kuisugua ili ahakikishe kama ni yenyewe.
“Binti sasa hivi umeamua kutoa original hahaha, lakini sijaelewa uneipata wapi hii azina kwa sababu hii ilikuwa inahifadhiwa kwenye jumba la gavana, wewe ni nani haswa mrembo?…._ Aliongea Aboku akimtwzama wonder machoni………
*******************************************************************************
Rest in peace marehemu .
Je ni nani atakaye kufa ……
General Ramos maskini …..
PENZI LA KIKOMANDO
EPISODE YA 05
MZIGO UMEFIKA GENERAL RAMOS KAZUA BALAA
TULIPOISHIA…..
Muacheni aende nitawapa Gold key original….” Aliongea wonder alipoona James anakabwa .
“Ipo wapi hiyo Gold key original au unataka utuchezee kama mwanzo?……”Aliongea Aboku akiwa amemuachia James na kumsogelea wonder.
Wonder anaingiza mkono wake nyuma ya mfuko wa suruhali yake na kutoa Gold key.
“ Hii apa mfungueni James ….” Aliongea wonder akiwa ameshika gold key mkononi .
Aboku kwa haraka sana anaichukua gold key mikononi kwa wonder na kuanza kuisugua ili ahakikishe kama ni yenyewe.
“Binti sasa hivi umeamua kutoa original hahaha, lakini sijaelewa uneipata wapi hii azina kwa sababu hii ilikuwa inahifadhiwa kwenye jumba la gavana, wewe ni nani haswa mrembo?…._ Aliongea Aboku akimtazama wonder machoni………
INAENDELEA…….
“Binti wewe ni nani haswa..” Aliuliza Aboku wonder akiwa anatetemeka kwa woga.
James akiwa bado yupo chini anaanza kuingiwa na mashaka baada ya kumuona wonder anatetemeka alipoulizwa yeye ni nani.
“Binti nijibu haraka wewe ni nani..? “ Aliongea Aboku kwa hasira akimpiga wonder kibao kilichotoa sauti kali.
“Ndio mimi ni mtoto wa general Ramos naapa nyie wapumbavu wote baba yangu lazima atawauwa na maiti zenu zitaliwa na wanyama…” Aliongea wonder kwa hasira akitokwa na machozi baada ya kupigwa kibao.
“Binti wa general Ramos….” Aliongea Aboku akiwa anatabasam.
James alishituka aliposikia wonder ni mtoto wa general Ramos.
“Ni kweli wewe ni mtoto wa general?….” Aliuliza James akiwa kama aamini alichokisikia.
“ Samahani sana James sikukuambia kabla ila ukweli ndio huo baba yangu ni general..”Aliongea wonder akitokwa na machozi wakiwa wapo chini ya ulinzi mkali.
“Kipeta huyu binti ni hazina kubwa sana kwa upande wetu mchuku tuondoke nae..”Aboku alitoa amri kwa muasi mmoja aliyeitwa kipeta.
Haraka sana kipeta anasoge na waasi wenzake watatu wanamshika wonder na kumnyanyua juu.
“Mwacheni huyo binti…” James aliongea kwa hasira akijaribu kukata kamba alizofungwa mikononi.
James anasimama kwa shida akitaka kumsaidia wonder mikono yake ikiwa imefungwa .
“James acha ujinga watakuuwa hawa, Mimi nitakuwa salama ondoa shaka…”Aliongea wonder akiwa amebebwa juu na kipeta . Lakini James hakutaka kuwa mpole aliendelea kuwasogelea waasi akitaka kupigana nao licha ya mikono yake kufungwa.
Aboku anachukua bunduki yake na kuielekeza mbele yake ambako alikuwa James amesimama.
“Hapana usifyatue…..” Wonder aliongea kwa sauti ya juu alikini Aboku hakutaka kusikiliza kelele ya wonder , Aboku anafyatua risasi inayoenda moja kwa moja mpaka upande wa kulia wa kifua cha James.
“Aaa wonder nitakusaidia ..” aliongea James akishika kifuani akiendelea kusogea taratibu walipo waasi.
Abuku anaweka target na kufyatua risasi nyingine mbili ambazo zinaenda upande wa kulia wa kifua cha James.
Wonder anabaki akitamzama James anavyoenda chini, macho ya wonder yanashindwa kuamini kitu kitu kinachoonekana mbele, wonder anabaki akitabasam kwa uchungu macho yake machozi yakiwa yametawala eneo kubwa.
Waasi wakiwa wamembeba wander juu wanaanza kuondoka nae eneo lile .
“Nitakumiss afande kijana …” Aliongea wonder akijawa na machozi uso mzima akiwa anatazama nyuma kulipo kuwa na mwili wa James
“Mkuu ule mwili wa yule jamaa situngeufukia tu?…..” Aliuliza kipeta ambaye ni msaidizi wa Aboku akiwa amembeba wonder wakiwa wanaondoka eneo lile.
“Huache uliwe na wanyama pori …” Aliongea Aboku akiwa anaendelea kutembea mkononi mwake akiwa ameshika gold key.
“Lazima na nyie mtakufa tena vifo vyenu vitakuwa vibaya kama wadudu… “ Aliongea wonder akiwa analia baada ya kusikiliza mazungumzo ya kipeta na Aboku.
“Kipeta mtulize huyo binti aache kutupigia kelele …”
“Sawa kiongozi.. “ Aliongea kipeta akiwa anamshusha wanda kutoka juu .
“We binti huwezi kufumba mdomo wako huu..”kipeta aliongea akiwa ameubana mdomo wa wonder kwa nguvu.
Wonder anaung’ata mkono wa kipeta kwa hasira
“Ayaaaaaaa mkuu nisaidie …” Alipiga kelele kipeta akiwa anajaribu kuvuta mkono kutoka mdomoni mwa wonder.
Aboku anarudi nyuma alipokuwa kipeta na kumpiga wonder kwa nguvu kwa kutumia kichwa cha nyuma cha bunduki, hapohapo wonder anapoteza fahamu na kudondoka chini.
“Mpumbavu mkubwa wewe, unashindwa maarifa na mwanamke, aya ubebe mwili wake tuondoke …” Aliongea Aboku kipeta akiwa anainama kuokota mwili.
DAKIKA 20 BAADAYE.
Jeshi likiongozwa general Ramos linafanikiwa kuvuka mlima na kuingia upande wa pili.
“Ongezeni mwendo mpaka mwanangu apatikane… “Aliongea general Ramos akiendelea kukimbia na kundi kubwa la Askari.
“Mkuu milio ya risasi ilisikika huku…” Aliongea Jordan ambaye ni mlinzi binafsi wa general Ramos akionyesha upande wa kushoto.
“Haya ongezeni mwendo..” aliongea general akiwa anaelekea upande wa kushoto.
Hatimaye wanafika sehemu ambayo wanakutana na nyayo nyingi za viatu.
“Zungukeni hili eneo mkague inaonekana waasi walipita hapa…” Aliongea general Ramos akiwa anakagua chini.
Mbele yake kidogo anakiona kiatu cha mwanae
Kikiwa kwenye tope.
“hiki ni kiatu cha binti yangu.. “ aliongea pekeyake kwa mshangao Askari wengine wakiwa wametawanyika wanafanya msako lile eneo.
Ghafla Kuna kelele ya Askari anaisikia upande wa pili.
“Jamani nimeuona mwili wa kaptain huku…” Aliongea askari mmoja kwa sauti kubwa akiwaita wenzake.
Askari wote walikusanyika pale na kuuna mwili wa James ukiwa umetapakaa damu nyingi.
“Pisheni…..”aliongea general Ramos akikatiza katika ya Askari kuelekea mpaka kwenye mwili wa James mkononi akiwa na kiatu cha mwanae.
“Ameshakufa?…”Aliuliza general Ramos alipomuona Jordan anaukagua mwili.
“Bado hajafa kabisa mapigo yake ya moyo yanapiga…” Aliongea Jordan akiwa ameweka mkono juu ya kifua cha James.
“James amka niambie binti yangu yupo wapi..” Aliongea general kwa hasira baada ya kugundua James bado anahema.
James anajitahidi kuongea akiwa yupo kwenye hali mbaya .
“Samahani kiongozi sikujua kama ni mwanao wameo…o…o..ndo…k…” Aliongea James kwa shida akielekezea mkono wake njia waliyopitia waasi Kisha akapoteza fahamu kabla hata hajamaliza kuongea.
“Pumbavu ,haya wote twendeni huku …”
General Ramos na askari wengine wakaanza kuelekea njia ambayo walielekea waasi mwili wa James ukitelekezwa pale pale chini.
General na askari walitembea umbali mrefu bila mafanikio yoyote.
“Watakuwa wamepita wapi sasa…” Aliongea general kwa hasira akipiga ngumi mti uliokuwa pembeni yake.
“Mkuu turudi tu tukiendelea kwenda mbele zaidi itakuwa ni kazi bure na hatari kwa maisha yetu…” Aliongea Jordan akiwa anasogea karibu na general.
“Rammmmmmm lazima nitakuuwa kama utamdhuru binti yangu…” General alipiga kelele kwa hasira na kuanza kurudi kambini yeye na askari wengine.
KAMBINI KWA WAASI
Ni katikati ya milima ambapo Kuna kambi kubwa ya waasi .
Ukatili mkubwa unafanywa ndani ya ngome hiyo kuna watu wengi wanaonekana kuteswa na wengine tayari wakiwa wameuliwa.
Aboku na wenzake wanawasiri kambini wakiwa wamebeba mwili wonder akiwa amepoteza fahamu.
Jeshi la waasi lililo baki ndani ya ngome linawakiribisha wenzao kwa kelele za ushindi.
“Kipeta nenda kamuweke huyo binti vyumba vya mateka ngoja nikaonge na Kiongozi….” Aliongea Aboku akiwa anaingia ndani.
“ Nimesikia kelele za furaha nje inaonekana umerudi na ushindi Aboku, mmewamaliza Askari wa general Ramos?…” Aliongea Ram ambaye ni Mkuu wa ngome ya waasi akiwa amevalia kinyago(mask) nyekundu usoni.
“Ndiyo mkuu , ushindi ni wetu siku zote kilichobaki ni kummaliza general Ramos tu maana binti yake tayari tunae na kikubwa zaidi ametupatia gold key…”Aliongea Aboku akiwa ameinamisha kichwa chini kuonyesha uheshima.
“Hahaha hatimaye leo nimempata binti yake, nitamuuwa kama ambavyo baba yake alivyoyauwa maisha yangu ….” Aliongea Ram akiwa anacheka na Kisha anarudisha kumbukumbu yake miaka Ishirini iliyopita.
MIAKA ISHIRINI NYUMA
General Ramos na Ram ni marafiki sana wanafanya kazi katika kikosi kimoja jeshini.
“Oya mshikaji unajua nampenda sana Maria sema tu naogopa kumwambia…” Ram alimwambia Ramos wakiwa wapo wanafanya mazoezi ya kulenga shabaha.
“Acha woga we mwanaume wa shoka unaogopa kumwambia mwanamke kama unampenda..”
“Hahahaha wewe mbona ulitumia mwaka mzima kumtongoza janeth alafu unanisema Mimi…” Aliongea Ram akiwa anacheka mkononi akiwa na bunduki aliyokuwa analengea shabaha.
******************************************************************
Kumbe General Ramos kiongozi wa jeshi na Ram kiongozi wa waasi walikuwa ni marafiki walioshibana sana!!!
Nini kilichopelekea Ram kuwa Muasi?
Kumbe Maria mke wa general Ramos kwa sasa zamani alikuwa anapendwa na Ram!!
MAMBO NI MOTO SANA
PENZI LA KIKOMANDO
EPISODE 06
MARIA KUFUNGA NDOA NA RAM!!!
TULIPOISHIA….
“Oya mshikaji unajua nampenda sana Maria sema tu naogopa kumwambia…” Ram alimwambia Ramos wakiwa wapo wanafanya mazoezi ya kulenga shabaha.
“Acha woga we mwanaume wa shoka unaogopa kumwambia mwanamke kama unampenda..”
“Hahahaha wewe mbona ulitumia mwaka mzima kumtongoza janeth alafu unanisema Mimi…” Aliongea Ram akiwa anacheka mkononi akiwa na bunduki aliyokuwa analengea shabaha.
ENDELEA……
“Acha zako unadhani janeth alikuwa mrahisi rahisi kama unavyofikilia, nimetumia nguvu kubwa pale…” Aliongea Ramos akiwa anaweka target sehemu ya shabaha mara Kuna sauti ya kike inasikika nyuma yao.
“Mpenzi nimekuletea chakula maana naona umegoma kabisa kurudi nyumbani, umeng’ang’ania kwa rafiki yao leo..” Alikuwa ni janeth ameshika kifungashio mkononi.
“Karibu nyumbani shemeji, lakini hicho chakula ulichomletea Ramos na mimi nakula…..” Aliongea Ram akiwa anaweka siraha chini.
“Hahahaha mke wangu usinge leta huku umeona sasa huyu jamaa na yeye anataka kula tukimwambie aowe anaogopa..” aliongea Ramos akiwa anasogea sehemu aliyokuwa mkewe.
“hahaha, acha uchoyo bwana kula na rafiki yako…” Aliongea janeth akifungua kifungashio kilichokuwa na chakula.”
“Shemeji ndio maana nakupendaga aise…” Aliongea Ram akisogea karibu na chakula na kuanza kula pamoja na Ramos.
“Mme wangu kipenzi ngoja mi niende ila hakikisha uchelewi kurudi nyumbani ….”
“Hakuna tatizo mke wangu naanzaje kuchelewa sasa!…”
Aliongea Ramos akiwa anaendelea kula chakula.
Janeth anaondoka nyumbani kwa Ram anamuacha Ram na Ramos wanakula chakula.
“Mmh mshikaji umepata mke mzuri sana hadi nakuonea wivu!..”
“Hahaha leo lazima twende kwa maria ukamwambie ukweli kama unampenda nimechoka unavyonisifia…”
“Kweli mshikaji lazima leo nikamwambie hisia zangu kwake maana daah kuishi hivi nimechoka….” Aliongea Ram wakiwa wamekaa chini na Ramos wanaendelea kula.
Wanamaliza kula moja kwa moja wanaanza safari kuelekea kituo cha watoto yatima ambapo anafanyia kazi Maria .Wanafika kituoni wanamuona Maria nje ya kituo akiwa anacheza na watoto.
“Haya sasa nenda kamwambie ..”
“ Ngoja leo nijikaze kama mwanajeshi, wewe baki hapahapa utazame mchezo….” Aliongea Ram akiwa anachomekea vizuri gwanda lake la kijeshi na kuelekea alipokuwa Maria.
“Afande Ram karibu jamani…” aliongea Maria alipomuona Ram anaingia ndani ya kituo.
“Watoto hamjambo?….”
“Shikamoo mkuu ….” Watoto wote walimjibu Ram.
“Marahaba haya nendeni mkapumzike ngoja niongee na Aunt yenu….” Aliongea Ram kwa ucheshi sana na watoto wote wakaingia ndani .
Ram akaenda kukaa na Maria pembeni kidogo ambapo kulikuwa na bembea .
“Ulitaka kusema nini afande?..” Aliuliza Maria akiwa amekaa juu ya bembea Ram akiwa amesimama .
“Usiniite afande bwana niite tu Ram inatosha…” Aliongea Ram kwa kutabasam.
“Ram..”
“Ndiyo…”
“ Haya niambie sasa jambo lililo kuleta hapa…”
“Aaaa ukweli….. Ukweli, Mimi hapa Maria …. Yani mimi hapa Ram ni ……” Aliongea Ram kwa woga akishindwa kumalizia sentensi yake Ramos akiwa anatazama kwa mbali anacheka.
“Unanipenda si ndio…” Aliongea Maria akiwa anatabasam.
“Ndiyo ….” Alijibu Ram Akitabasam baada ya kuona Maria anafuraha
“Unajua wewe ni muoga sana yani nilijua mda mrefu kama unanipenda nilikuwa nasubiri tu useme, sasa kwa nini umechelewa kuleta posa kwa wazazi wangu?….” Aliongea Maria kwa kutabasam.
“Kwani na wewe unanipenda? ..”aliuliza Ram akiwa anasubiri jibu kwa hamu.
“Ndiyo nakupenda…”alijibu Maria
“Ramosiiiiiiiiii mpango umetiki…”
Alipiga kelele Ram kwa sauti akimwambia Ramos aliyekuwa amekaa mbali kidogo na pale lakini Ramos hakuongea kitu aliondokasura yake ikiwa na hasira ishara ya kutopenda kitendo cha Ram kukubaliwa na Maria.
“He wewe kumbe ulikuja na Rafiki yako!…” Aliongea Maria baada ya kumuona Ramos kwa mbali akiwa anaondoka.
“Ndiyo nilikuja nae lakini aijui kwa nini anaondoka ….” Aliongea Ram akiwa bado anafuraha za kukubaliwa na Maria.
Siku chache baadae Ram alijiandaa na kwenda kwa wazazi wa Maria kutoa posa.
Wazazi wa Maria hawakuwa na kipingamizi chochote sababu hata binti yao aliridhia kuolewa na Ram.Maria na Ram kwa pamoja wanapanga ndoa yao ifanyike siku tano mbele wazazi wa Maria wanaridhia jambo hilo kwa furaha.
“ Ukimuoa binti yangu usije ukaanza kumfanyia majaribio ya mazoezi yenu ya jeshi…” Aliongea baba Maria kwa utani akiwa amekaa na Ram.
“Hahahaha siwezi kufanya hivyo baba….” Aliongea Ram akiwa amemshika Maria mkono.
Ram alienda mpakanyumbani kwa rafiki yake Ramos na kumwambia kuhusu harusi lakini Ramos hakuonekana kuwa na furaha.
“Changamka basi mshikaji mbona umepoa hivyo…” Aliongea Ram akiwa anampigapiga Ramos.
“ Shemeji wangu huyo anaenda kuwa mme……” Aliongea Janeth akitokea ndani akiwa ameshika chakula.
“Ndiyo shemeji zimebakia siku nne tu na Mimi naanza kupikiwa
Kama rafiki yangu hapa….” Aliongea Ram kwa furaha sana Ramos akawa anatoa tabasam la kujilazimisha.
Ram na Ramos wakiwa wapo pale ghafla kunaujumbe unawafikia inatakiwa wafike kambini haraka.
Bila kuchelewa wanafika kambini na kukutana na wenzao.
KAMBINI
“ Nini kinaendelea hapa, mbona watu wametumwa kutuita sisi…”
Ram aliwauliza wanajeshi wenzake aliowakuta wamekaa kwenye mstari wakimsubiri general.
Mda huohuo General anaingia akiwa na viongozi wengine, jeshi lote linapiga salute kutoa heshima kwa general. General anasogea mpaka kizimbani na kuanza kuongea.
“Jamani kunataarifa mbaya tumezipata ni kwamba nchi yetu inaelekea kuvamiwa na kundi la SK ambalo lipo milimani linakuja sasa bila kupoteza mda inatakiwa twende tukawadhibiti kabla hawajaingia kwenye makazi ya raia, …..” Aliongea general kwa sauti kubwa akiwa kizimbani.
INAENDELEA……
KUMBUKA BADO TUPO KWENYE HISTORIA YA MIAKA 20 ILIYOPITA
*Vita kali sana kati ya Askari na kundi la SK
*Usikose sehemu ijayo ya hii simulizi**