Clickable WP Image

JOIN US WHATSAPP CLICK HERE
JOIN US TELEGRAM CLICK HERE

 SABABU ZA MWANAMKE KUPOTEZA HISIA ZA
MAPENZI


Mwanamke anaweza kupoteza hisia za mapenzi kwa sababu zifuatazo:


1. MAUMBILE
Mwanamke anaweza kupoteza hisia za mapenzi kwa sababu ya kupata maumivu makali
sana wakati wa kujamiana ambapo vyanzo vinaweza kuwa kusumbuliwa na magonjwa
mbalimbali kama saratani, arthritis, kisukari, shinikizo la damu,ugonjwa wa
moyo,na magonjwa ya neurology

vilevile vyanzo vingine ni matumizi ya dawa kali kama vile baadhi ya
antidepressants hushusha chini hamu ya tendo la kujamiana.

-Mitindo ya maisha inaweza pia kuathiri hisia za mapenzi kama vile unywaji wa
pombe kupindukia, matumizi ya dawa za kulevya,uvutaji sigara kupitiliza
husababisha kushuka kwa kasi mzunguko wa damu mwilini hivyo huathiri sana hamu
ya tendo la kujamiana

vilevile matibabu yenye kuhusisha upasuaji wa matiti au viungo vya uzazi
huathiri sana hamu ya tendo la kujamiana.

2. HOMONI
Mabadiliko ya homoni pia yanaweza kuathiri sana hamu ya tendo la kujamiana kwa
mwanamke ,umri pia huathiri sana hamu ya tendo la kujamiana hasa pale ambapo
mwananmke anapofikisha umri wa miaka 45+ hasa pale ambapo mwanamke anapofunga
kupata hedhi.

vilevile hedhi kuvurugika mara kwa mara inaweza kuathiri sana hamu ya tendo kwa
sababu baadhi ya wanawake wakikaribia hedhi huwa wanapata maumivu makali sana
chini ya kitovu.

Hivyo hedhi kuvurugika mara kwa mara husababisha mwanamke anakuwa na hasira
kupitiliza,ubabe, kujichukia,kumchukia mwanaume bila sababu.

Vilevile baadhi ya wanawake husumbuliwa na tatizo la ukavu sehemu za siri kwa
maana hakuna yale majimaji ambayo hulainisha sehemu ya uzazi ya mwanamke ambayo
huwa kama kilainishi wakati wa kujamiana.Ule ute ute wa kwenye njia ya uzazi
unapokauka husababisha michubuko wakati wa kujamiana ambapo husababisha
Mwanamke anakuwa mkali kupitiliza wakati wa tendo jambo ambalo husababisha
ugomvi wa mara kwa mara wakati wa kujamiana.

3. MATATIZO YA KISAIKOLOJIA
Mwanamke anaweza kupoteza hisia za mapenzi,kukosa hamu ya tendo la kujamiana
kwa sababu ya Stress kupitiliza kwa mfano kuzongwa na mawazo kwa sababu ya
-Ugumu wa maisha,madeni sugu,uchovu wa kazi za kutwaa nzima,kuuguza wagonjwa,
kuhudumia watoto wenye kusumbua sana kutwaa nzima, kuhudumia mzazi mzee sana,
vilevile kunyonyesha husababisha baadhi ya wanawake kupoteza hisia za mapenzi.

vilevile baadhi ya wanawake hupoteza hisia za mapenzi kwa sababu anakuwa na
huzuni kupitiliza labda anakuwa amepata msiba wa mpendwa wake,au migogoro ya
kifamilia ya mara kwa mara,

vilevile Mwanamke anaweza kupoteza hisia za mapenzi kwa sababu ya kupewa ahadi
hewa mara kwa mara,hofu ya usalama wake,

mwanaume kukosa lugha nzuri ya kubembeleza penzi husababisha mwanamke anapoteza
hisia za mapenzi kwa sababu anakuwa kama anabakwa.

pia manyanyaso kutoka kwa mwenza wake kama vile kupigwa,kufokewa, kutukanwa,
kujibiwa vibaya, kudhalilishwa mara kwa mara, kutolewa dosari za
muonekano,kuambiwa “Hauna akili” mara kwa mara,kuambiwa “unanuka
sehemu za siri usiniguse”,,wengine huwa wanapitia vipigo vikali sana kila
siku kabla ya kujamiana kwa maana ya kuingiliwa kinguvu.

Pia kumbukumbu mbaya zenye kuhuzunisha kama vile kubakwa, kulawitiwa,njia ya
uzazi kutanuka sana baada ya kujifungua husababisha mwanamke anajichukia sana
hivyo anapoteza hisia za mapenzi,baadhi ya wanawake huwa wanajichukia sana kwa
sababu ya muonekano hivyo huathiri sana hisia za mapenzi.

Share.
Leave A Reply

error: Content is protected !!
Verified by MonsterInsights