isiyomaanisha, akiwa kwenye mwonekano unaoitwa seriously.
Kisha akabadilika kuwa kwenye huzuni ya kweli, kama utaamua kukubaliana na
yeye.
Kwasababu alihitaji umbembeleze, sio utembelee kauli yake.
Ngoja nikwambie kitu mwanaume mwenzangu.
Siku mojamoja kuwa Kaisal kimaandishi, halafu msomee kwa sauti ya Khan Mbarouk.
Mwambie licha ya udhaifu wako wa kutamani wengi, lakini unampenda peke yake.
Msimulie hadithi za kina Sharifa na Sarah, walioahidi kukupa hadi Mungu
alivyovikataza.
Mwambie amestahili kuwa na wewe, sio bahati kama mitaa inavyozungumza.
Mkumbushe sifa ulizomwongopea, kipindi cha harakati zako za kumtongoza.
Mwambie unamwona malaika aliyetoroka peponi, kila unapomtazama Eva wako wa
Vikindu.
Mfanye ajione special sana kwenye hii dunia, mwambie hauna maisha
yanayoeleweka, kama ataamua kuishi mbali na wewe.
Wakati mwingine tunawapoteza wa ndoto zetu, kwa kufeli course nyepesi ya
kuelewa hisia zao tu.
Mpe kitu cha kujivunia ndani ya moyo wake, tofauti na tukio la kumheshimisha
ngariba wako.
Mwanamke ni kama uyoga, sumu yeye, chakula yeye, wako jitahidi umwelewe.