1. Unaleta pesa ya matumizi nyumbani.
Moyo wa mwanamke utachoka kukupenda iwapo utaacha kuleta hela ya matumizi
kwa ajili yake na watoto nyumbani.(Women are materialist in nature!), wao ni
watu wa kupenda vitu sanaa kutoka kwa mwanaume na ndiyo upendo wao na heshima
kwa mwanaume wanavyoutafsiri. Usipompatia pesa kwa ajili ya matumizi yake na
watoto, ndivyo atakavyozidi kukudharau siku hadi siku atafika hatua atakukinai
vibaya sana, kiasi kwamba anaweza kutamani kukupa nguo zake za ndani
umfulie.KWANINI? ATAKUSHUSHA HADHI YA UANAUME, MWANAUME LAZIMA AKUBALI KUBEBA
MAJUKUMU YA KUHUDUMIA FAMILIA. Upate, ukose wao hawajui! Wanachotaka wewe
uhudumie na kutunza familia tu!. UTAPATAJE PESA, hiyo inabaki juu yako! Kama
mwanaume unalelewa na mwanamke, tambua kwamba heshima yako haipo, kuna siku
atakuchukulia wewe kama mfanyakazi wake wa ndani na sio MUME WAKE, SIKU ZOTE
MAPENZI YA KULELEWA NA MWANAMKE HAYADUMU. Anza sasa kujenga heshima yako kwa
kuacha CHOCHOTE MEZANI.
2. Ni mtu wa ibada na kusali sanaaa.
Aisee, church boys( wanaume wanaopenda kusali) wanapendwa sana na wake zao.
Why? Kwasababu wanaamini sio watu wa mambo mengi hasa ya kupenda wanawake,
ulevi na starehe nyingine ambazo zinaweza kusababisha ndoa ikavunjika. Kiufupi
watu wanaosali sana wanaaminika sana ndani ya ndoa ndiyo maana hata wakati wa
kuoa watu wanapenda sana kuchagua mke au mume kutoka kwenye nyumba za ibada.M
WANAUME
ILI UANZE KUPENDWA NA MKE WAKO, KAMA AMEPOTEZA IMANI NA WEWE, ACHA MAKANDO
KANDO YAKO NA ANZA KUSALI KWA SANAA! HAKIKISHA HAUKOSI IBADANI, LAZIMA
ATARUDISHA IMANI NA MAPENZI KWAKO.
3. Una nguvu za kiume(WEWE NI MWANAUME KAMILI)
Aisee, iwapo jogoo wako hawiki, iwapo huwezi kushiriki tendo la ndoa,mke
wako atakushusha thamani na anaweza kukuacha kabisaa. Kwanini? Kwasababu kuwa
mwili mmoja kuna kamilishwa na tendo la ndoa, kama hamshiriki tendo la ndoa,
maana ya mwili mmoja INAPOTEA na kubakia kwenye makaratasi ya vyeti vyenu vya
ndoa pekee. Wapo wanaume walipata ajali wakapoteza uanaume wao, wapo ambao
wameugua wakapoteza uanaume wao lakini hawajaachwa na wake zao, nawapongeza
sana wanawake wa aina hiyo maana wana imani kubwa. INAHITAJI UPENDO, IMANI KWA
MUNGU NA KUMTEGEMEA SANA MUNGU ILI AKUPE UJASIRI WEWE MWANAMKE WA KUMLINDIA
MUME WAKO HESHIMA YAKE MPAKA HATUA YA MWISHO YA MAISHA YENU. Sio rahisi
kwasababu sote ni binadamu tumeivaa miili yenye tamaa za kimwili kibaiolojia
lakini peke yako hauwezi isipokuwa kwa msaada wa Mungu. WANAUME TUNAPASWA
KULINDA UANAUME WETU KWA NGUVU ZOTE ILI HESHIMA YA NDOA ZETU IWEPO
TUSIDHARIRIKE. TUTALINDAJE UANAUME WETU? KWA KUACHA KUJICHUA, KUACHA KUTAZAMA
PICHA ZA NGONO,KWA KUACHA VINYWAJI VIKALI, SIGARA, VYAKULA VYA MAFUTA, KWA
KUFANYA MAZOEZI LAKINI PIA KWA KUMTEGEMEA MUNGU MAANA KUACHA KUJICHUA, POMBE NA
SIGARA SIO RAHISI PASIPO MUNGU.
4. Unamshirikisha kwenye maamuzi yako.
Aisee, kama unamshirikisha mke wako wakati wa kufanya jambo lolote basi
wewe unaijua maana ya ndoa. Hupaswi kuamua mambo yote mwenyewe kwasababu wewe
ni mwanaume, hapana! KWANINI? KWASABABU KUNA LEO NA KESHO. Ukiamua mwenyewe
tena kwa siri pasipo mke kufahamu, utaondoka na kuacha mali zingine
hazifahamiki, watoto wako wataishi maisha ya kimasikini huku wanafaidi jasho
lako watu wengine kabisaa. NDIYO MAANA WANAWAKE WANAWAAMINI NA KUWAPENDA SANA
WAUME ZAO WANAOWASHIRIKISHA KWENYE MAAMUZI HASA YA UCHUMI WA FAMILIA