Monday, April 28, 2025

Wasichana Angalieni haya Mambo 12 Mabaya Kabla Mwanaume Hajakuoa

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


 Mambo 12 Mabaya Wasichana Angalieni Kabla Mwanaume Hajakuoa


Wanawake wengi wanajulikana kwa msingi wa maamuzi yao ya ndoa juu ya mambo ambayo hayatadumu maishani. Haya makosa wameyafanya wengi wao kuingia kwenye ndoa zisizo sahihi na kugeuka kuwa watumwa wa maisha ya ndoa. Tunahitaji kutambua na kukabiliana nayo:

1) UREFU:
Ndoto ya kila msichana leo hii duniani ni kuolewa na mvulana mrefu, mweusi mwenye sauti ya baritone, nashangaa walipata wapi wazo la kuwa wavulana warefu ni bora zaidi kuliko wengine kwenye ndoa. Halo Wasichana, mtu mrefu anaweza kukupa shida ndefu; urefu sio kitu muhimu lakini cha mhimu mtu awe na kina cha utu na ubinadamu katika kumcha Mungu na tabia tabianzuri.

2) MISULI:
Wavulana wenye sura ya misuli na miili mikubwa maarufu kama vidali pia hawa nao wana bahati kwenye ulimwengu wa ndoa, wanaonekana kuwa wachumba wazuri, na wasichana husema wanaonekana wanaume. wanaonekana kama wanaume halisi. Poleni sana Wasichana, misuli haifanyi mwanaume awe halisi, na mwenye uhusika na uwezo wa kubeba majukumu kama mume. kwasabau Mvulana akiwa na misuli bila kuwa na tabia njema atatumia misuli yake kukabiliana na wewe na kila siku badala kukulisha chakula kizuri uzidi kunawili atakulisha kipigo mwisho atabaki kama mbwa koko uliyekosa mfugaji na kuharibu uzuri wako.

3) NYUMBA NZURI:
Mvulana mwenye nyumba nzuri basi mvulana huyu ni ndoto ya kila msichana. Wasichana wengi watatupa shida sana upeo wao mfupi ni kuwa na mwanaume aliyejenga nyumba yenye ukubwa wa ikulu ya Mfalme; yenye Seti nzuri za Kiitaliano, jiko la umeme, friji lenye vinywaji vingi, ukumbi wa michezo wa nyumbani, jokofu, jiko la gesi, Plasma TV, kitanda 6 kwa 6, Jikoni, meza ya dining, mashine ya kufuria, washer wa sahani, n.k. kwa wasichana wenye mawazo haya Poleni sana, nyumba iliyowekwa vizuri ni nzuri kweli lakini kuna muda nyumba hii hubadirika na kuwa shida iliyopambwa vizuri ikiwa mvulana sio mtu mwenye tabia njema na mcha mungu huko adabu naa busara, ataifanya nyumba iwe kama uwanja wa gereza kwenye maisha yako.

4) AKAUNTI YA BANK:
Wasichana wanapenda kuwa na mvulana aliye na utajiri kwa kumuangalia akiwa na simu nzuri na account za benki. wasichana wanaamini kuwa wataishi maisha ya furaha kuolewa na mvulana mwenye pesa hasa pale wakati wanapogundua kuwa mvulana huyo ni tajiri sana. wasichana Hawataki kujua pesa na utajiri huyu bwana unavitoa wap hata hawataki kujua huyo jamaa anafanya kazi gani. Kinachowahusu wasichana ni pesa zinazopatikana kwa wakati huo ni kutumia tu. kuna Wasichana wengi waliishia kujikuta wameingia kwenye maisha ya aina hii lakini wakageuka kuwa watumwa wa ndoa zao kuna wakati pesa hii hugeuka udhaifu kwako na mwanaume akakufanya atakavyo hata kuleta mwanamke mwingine chumbani kwako, usiweke ndoa yako iwe kwenye CHOYO, ndoa yako itageuka kuwa nyekundu kama bahari ya damu.

5) MAHALI PA KAZI:
Baadhi ya wasichana wetu wana mazoea ya kufanya maamuzi ya ndoa kulingana na mahali ambapo mvulana anafanya kazi. Huthubutu kuwatamani kuhusu ndoa hasa ikiwa wewe ni Mwalimu au mtumishi wa serikali. Huwezi kuwaksa wadada wenye ndoto za kuolewa na wafanya kazi za serikali lazima wajipendekeze lakin ukifanya kazi ndoto hutawaona hao, au biashara ya mtu ndogo. usiombe Wasichana wagundue kuwa, mvulana anafanya kazi ACCESS BANK haimaanishi kuwa mwanaume wa namna hiyo atakupa upendo wa moyo wake au utulivu wa akili. Mvulana anayefanya kazi SHELL anaweza kufanya maisha yako yakawaka moto kama SHELL iliyolipuka milele, wewe sio wa KWANZA katika maisha ya kijana anayefanya kazi BANK kuna wenzio 30 walipotea njia kama wewe leo na upeo wako mfupi, kijana anayefanya kazi BANK hawezi kukuhakikishia maisha yako ya baadaye akiwa anamaanisha toka moyoni. Anaweza kuwa anafanya kazi NESTLE lakini asiwe MTULIVU nyumbani, Kwa hiyo ndoa haihusu anafanya kazi wapi bali ni nani anayemaanisha kutoka moyoni kwenye ndoa yake kumbuka kuna anayefanya kazi inayobarikiwa na mikono ya mungu na yule anayefanya kazi kwa kushirikiana na shetani.

6) UPENDO:
Mwanadada mmoja alisema, Mvulana huyu anamvuto wa kimapenzi, wamoto na mtanashati, nitaolewa nae. Dada acha mawazo hayo, Mapenzi pekeake hayatoshi kuwa ndoa. Ukweli ni kwamba, watu wengi wanaoitwa wavulana wenye mvuto wa kimapenzi huwa hawabaki njia kuu hasa ikitokea wamesifiwa hata wakioa. Olewa na mvulana kulingana na sifa ambazo zitadumu milele, mapenzi huwa hayadumu milele ila ndoa huwa inadumu sasa ukitaka kudumisha mapenzi kwanza dumisha ndoa, nenda kaulize wanawake waliokutngulia kuolewa.

7) MAGARI:
Wasichana wengi watashawishiwa na mvulana anayeendesha gari kubwa na la gharama kubwa. Wengine hawana ndoto za kuwa na mtu ambaye hana gari. Ikiwa unataka kujisumbua na ukose kupata wadada wazuri basi panda au endesha baiskeli kwenda siku ya kwenda kumchumbia mwanamke unayempenda, utasikia. Wanawake wakisema kama kaja na baiskeli ujue wewe utaishia kwenye mkokoteni, lakini ukweli ni kwamba kijana ambaye ana GARI anaweza ASIKUJALI kabisa, kwababu maisha sio GARI, ni kuolewa na mtu ambaye ATAJALI maisha yako ya baadaye.

8. PASPOTI
Wasichana wengi wanaolewa kwa urahisi na mtu yeyote aliye na pasipoti za Marekani au Uingereza, Wasichana wengi wameharibu maisha yao katika harakati za kutafuta mtu mwenye pasipoti ya kigeni wanaamini ndiye anayefaa kuoa.

9) UIMBAJI NDANI YA KWAYA:
Inachekesha baadhi ya wanawake wapo tayari kuolewa na baadhi ya wavulana kwa sababu ni wazuri sana kwenye kuimba kwaya, au wale wanaoweza kupiga Sax foni, keyboard, ngoma, tarumbeta na kuimba tenor na kupiga gitaa la Bass vizuri sana. sijui kama wanataka kuanzisha bendi ya kwaya katika nyumba zao.

10) WATOTO WA MATAJIRI:
Watoto wenye wazazi Tajiri ni walengwa rahisi sana kwa wasichana wengi wachanga si kwa sababu wanapendana nao hapana, ni kwasababu wanajua watapata pesa kwenye uhusiano huo. Wengi wa wavulana hawa wanaotoka katika malezi tajiri ni watu wa kustaajabisha sana, wanakuwa wajanja, wenye majivuno na huwa wanakuwa waume na baba wabaya na wasiowajibika kwenye majukumu yao lakini wasichana hata hawajali hilo, Wengi wa wasichana hawa huishi kwa kujutia uamuzi wao mbaya.
Usiolewe na mtu yeyote kwa sababu tu wazazi ni matajiri, oleweni
na mtu kwa jinsi alivyo na upendo wake wa kweli.

11) UONGOZI WA USHARIKA: Wanawake wengi wa Kikristo wako tayari kufa ili tu waolewe na ndugu walio katika wasimamizi wa usharika wao wa Campus za kidini. Wanapigana mpaka kuong'oa jino na kucha ili kupata usikivu wa ndugu hawa, wengine hufikia hatua ya kutoa miili yao. Wengi wa wanawake hawa wanafikiri kwamba wanaume bora kuliko wote ni watendaji wa Campus za kidini , wamesahau kwamba RAISI WA USHARIKA HUENDA ASIWE NA MAKAZI HUKO MBINGUNI.

12) UTAALAMU CHUMBANI:
Mojawapo ya njia ya kijinga zaidi ya kufanya uamuzi wa nani wa kuolewa nae wanawake huzingatia jinsi jamaa alivyo sura ya kuvutia au jamaa alivyokuwa bora chumbani. Ukiegemeza uamuzi wako wa ndoa kwenye uwezo wa kupiga show wa mwanaume; unaweza kujikuta unaishi kwenye ndoa na mwanaume play boy au malaya badala ya kupata Mume aliye bora. Unaweza kuishia kuolewa na mwindaji wa mademu, badala ya mpenzi wa kweli. Utaishia kuolewa na mgawaji wa mbegu za kiume kwa wanawake wote na mwanaume wa jinsi hii ipo siku atalala na dada yako, mfanyakazi wa ndani, marafiki zako wa karibu, wasichana wa jirani, sekretari wake na chochote kile kinachovaa sketi.

Add Comments


EmoticonEmoticon