Tuesday, April 29, 2025

Ukweli lazima Usemwe - Makosa ya Wanaume na Wanawake wa Siku hizi

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


 UKWELI LAZIMA USEMWE


1. Wanawake huwa hamjali mwanaume anayempenda na kumheshimu mama yake, mnachofanya ni kumuona kama akili ya kitoto au humuita mtoto wa mama fahamu kuwa kuwaheshimu wazazi wako hapa duniani ni daraja kubwa sana kuliko udhaniavyo wewe

2. Wanaume tumeshau uungwana na kuchukulia kawaida bila kujali kuwa mwanamke kuna muda anatakiwa anunuliwe make up na na avae vizuri, tunachofanya ni kumfanya mwanamke aonekane kama hana akili timamu na asiye na maana na kusahau kuwa anathaman kuliko mali tunazozikumbatia kikubwa unachotakiwa kufanya ni kumtunza na kuthamin umbile lake na mwili wake.

3. Kweli dunia imeisha kuna Wanawake siku hizi sijui wameibukia wapi wao hawajali waume zao hasa wale waume wanaopenda mpira au siasa, wanawake wanachofanya ni pale mwanaume anapokuwa yupo bize na siasa au mpira wao hukaa chini na kupanga mbinu za kutawala maisha ya waume zao ili tu wawe juu ya waume zao.

4. Wanaume hatujali mwanamke anapopata mafanikio zaidi, tunachofanya ni kutumia akili pale mwanamke akisha pata utajiri huwa tunafikiri kuwa pesa za mwanamke tuhaki nazo ya kuwa huwa tunaamini huenda kahongwa na bwana mwingine huwa hatuamini kuwa mwanamke naye anaweza kupambana na kuishia kuwadhalilisha wake zetu.

5. Wanawake huwa hawajali mwanaume anayejiamini kwenye maisha, wanachofanya ni pale ujasiri wa mwanaume unapochanganyikana na kiburi wao huwa hawezi kuamini kuwa anaweza kujirekebishwa au kusema samahani akikosea.

6. Wanaume huwa hatujali wanawake wanaopenda kutazama sana vipindi vya Televisheni na video za Instagram, maana wanawake hawa wanachofanya ni pale wanapojizima data na kutaka kuishi maisha kwa kukopi wanachokiona kwenye TV au mtandaoni.

7. Wadada wengi siku hizi hawajali wanaume zao hasa wakitaka penzi, wanachofanya kila siku siku visingizio visivyo na pua wala mguu.

8. Wanaume hatujali mwanamke anayekuwa na marafiki wa kike, tunachofikiri ni kwamba mwanamke huyo atakuwa anafichiwa siri zake za mahusiano yake na mashoga zake hasa kupeana siri za uhusiano/ndoa yake na kudanganywa jinsi ya kutembea na wanaue wengi.

9. wanawake hawajali mwanaume mwenye akili timamu na anayejielewa zaidi kuishia kupendana na vjana wahuni vijana wa hovyo

10. mume/mke wako leo hii hajali wewe kuwa una imani flani muislam/mkristo, mawazo ya mwenzi wako yanaweza kugeuza kila kitu kizuri cha neema kwenye ndoa/mahuiano kama kati yenu kuna mwenye imani na kumtazamia Mola

Add Comments


EmoticonEmoticon