Monday, April 28, 2025

Mambo 10 ya Kuzingatia - Ukiwa kwenya Mahusiano ya Kimapenzi

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


TIBA 10 BORA ZA MAHUSIANO

1. Upendo ni chaguo. unatakiwa kuwajibika kwenye chaguo lako. Hakuna asiyejua kupenda. Mapenzi na vivutio ni vitu viwili tofauti, unaweza kuvutiwa na mtu lakini mapenzi yakafifia mapema.

2. Furaha yako, utimilifu wa furaha unakutegemea wewe, kwa maana nyingine usiruhusu mtu yeyote kukuamulia furaha yako wakati wewe unapaswa kuwa na furaha yako kwaajili ya maamuzi yako, Kuwa huru kihisia. Usiwekeze hisia zako kwa mtu yeyote bila kumtambua vizuri, kumbuka kwenye chaguo lako unapaswa kuwajibika kfanya maamuzi yako mwenyewe

3. Kukabiriwa na changamoto. Watu wengi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika mahusiano/ndoa zao kwa sababu ya hadithi nyingi za uongo, kupitia filamu za Nollywood, Hollywood na Korean romance, kwanza mule kwenye filamu hakuna ushahidi maalum juu ya wanachigiza Kumbuka hawa watu wanaoigiza kwa kutumia script ya mtu, wakati mwingine huwa sio ukweli sasa bro, amka mapenzi hayafananishwi na sinema.

4. Jiulize
Kwa nini unataka kuwa kwenye mahusiano hayo?
Kwa nini unataka kuolewa/kuoa?

5. Mpende utakayefunga naye ndoa, jifunze kuendesha gari aina ya upendo katika mahusiano yako. Kumbuka, ukosefu wa mawasiliano sahihi huharibu mahusiano,

6. je huwa Unazungumzia nini katika mahusiano yako?
kila siku huwa unamwambia mpenzi wako maneno haya au ndiyo huyajuihebu mwambie maneno haya basi nakukumbuka au unakuja lini umemis kuniona au umekula? tafadhari kula kwa ajili yangu

7. Eleza maono yako, jadili ndoto zako, panga maisha yako ya baadaye na unayempenda.

8. Usifanye mahusiano yako kuwa Miungu wako, Daima tengeneza ratiba

9. Usisukumwe kwenye mahusiano yako na vitu unavyoviona. Ndoa au uhusiano hautasuluhisha shida zako, badala yake utakutana na shida zaidi ya hizo ulizonazo (kama una shaka soma 1 Kor 7

10. Hakuna mwanaume/mwanamke anayetaka kuoa dhima hivyo usijifanye kuwa mmoja. wakati mnatakiwa kuishi wawili


Kumbuka: Unawajibika kwa mustakabali wako kwa mwenyewe idhibiti wa maisha yako .

USITEGEMEE MTU KWA HISIA, FAHAMU SANA JUU YA HILO



Add Comments


EmoticonEmoticon