Tuesday, April 29, 2025

Sheria 12 Zitakazoongoza Ndoa yako - Vitu Muhimu vya Kuzingatia

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


SHERIA 12 ZITAKAZOONGOZA NDOA YAKO


AWatu wawili wanawezaje kuongozana pamoja wasipopatana? Ukweli ni kwamba, ndoa nyingi huharibika kwa sababu ya kutoelewana pande zote mbili. Kutoelewana kunaletwa ukosefu wa maelewano ya kushughulikia masuala yanayoathiri kila ndoa. Kushindwa kukubaliana kutapelekea mume na mke kutafsiri mambo kwa njia tofauti na kusababisha kuumiza hisia
Kubaliana na mwenzi wako kuhusu cha kufanya na usichofanya. Kuwa na sheria hizi.

1. SHERIA ZA TENDO LA NDOA
Kubali kwamba unaweza kufanya tendo la ndoa kwa njia yenye msimamo, lakini pia ukubaliane juu ya kile ambacho hautajaribu kufanya. Kwa mfano; hakuna ngono ya kinume na maumbile, au kutopiga punyeto unapokuwa na wenzako, au hamtumii filamu za ngono, kutofanya mapenzi wakati mwenzako yupo kwenye hedhi Kila wanandoa wanapaswa. Kukubaliana juu ya kuwa na mipaka

2. SHERIA ZA SIMU
Kukubaliana jinsi ya kushughulikia mambo ya simu. Kwa mfano, hakuna kuzungumza na watu wengine ifikapo saa 5 usiku kwa maana hiyo ni mida ya wewe kuwa karibu na mwenzio, na hakuna usiri, hakuna haja ya kuondoka na kwenda kupokelea simu, nje mjulishe mwenzi wako nani aliyepiga simu hiyo.

3. SHERIA ZA PESA
Kukubaliana jinsi ya kutumia pesa. Je, mtakuwa na akaunti ya benki ya pamoja? Ni asilimia ngapi kila mmoja anaweza kutumia bila hitaji la kumjulisha mwenzake? Nani wakulipa bili? Kuhifadhi. Kuwekeza. Hakuna kutoa pesa kwa wakwe bila ridhaa ya pamoja

4. SHERIA ZA KUJA NYUMBANI
Unapaswa kufanya nini ikiwa utachelewa kurudi nyumbani? Kupiga simu? Je, umechelewa kiasi gani kurudi nyumbani? Mwenzi wako hajali wewe kuchelewa kurudi nyumbani mradi tu wamekubali. Ndoa sio ubinafsi bali ni ninyi wawili mnapaswa kushiriki

5. KANUNI ZA KIJAMII
Kubali kutambulishana kwa marafiki zanu. Kubalianeni yakuwa na marafiki wa karibu wa jinsia tofauti. Kubaliana ni marafiki gani wanafaa kubaki kwenye maisha yenu. Kubalianeni ni mara ngapi marafiki wanaweza kuwatembelea. Nyumba kwenu haipaswi kuja kwa kuvamia na marafiki. Kuna haja ya kuwa na mipaka

6. KANUNI ZA HABARI
Kubalini kutarifiana mahali kila mmoja alipo, hata ikiwa kwa maandishi rahisi tu au meseji. Kubalianeni juu ya hitaji la kuambiana ratiba zenu binafsi kwa siku. kila mtu amjulishe mwenzie

7. KANUNI ZA HASIRA
Kubalianeni juu ya nini cha kufanya wakati nyote wawili mnapokuwa mmekasirikia. Je, unampa mwenzio nafasi? Ungependa kuondoka eneo la ugomvi kwa dakika kadhaa? Je, unashughulikia suala hilo haraka? Kila mmoja Hakuna kwenda kulala bila kuelewa na kupata mbinu ya Utatuzi wa migogoro yenu

8. KANUNI ZA KAZI NDANI
Kukubalianeni juu ya nani anafanya nini ndani ya nyumba. Hii itazuia yeyote kati yenu kuhisi kama anafanya sana kazi kuzidi mwenzio

9. KANUNI ZA MITANDAO YA KIJAMII
Kubalianeni juu ya mambo ya kufanya na yasiyofaa ya mitandao ya kijamii. Kwa mfano, kutokuwa na urafiki kwenye Facebook na mpenzi wako wa zamani, kutotoa maoni mitandaoni kwa njia ya kuchukiza kwenye chapisho la watu wengine, kutokuwa na tabia chafu, kutotangaza masuala ya nyumbani kwenye mitandao ya kijamii.

10. KANUNI ZA KAZI
Kukubaliana juu ya mipaka ya kazi. Kwa mfano, ukirudi nymbani usilete kazi za ofini kwako nyumbani, nini cha kufanya wakati kazi zako zinagongana? Nini cha kufanya unapokuwa na saa tofauti za kazi? Wakati wa kuchukua likizo au siku za kupumzika?

11. SHERIA ZA UZAZI
Kukubaliana jinsi ya kuwaadhibu watoto, nani anafanya nini, nani atawajibika maswala ya Wazazi shuleni, je! watoto watakula chakula cha aina gani?

12. KANUNI ZA NAFASI ZA MTU
Kubalini kwamba wakati fulani kila mmoja wenu atataka muda fulani awe peke yake, kufanya kazi au kutafakari au kupumzika tu. Kubali jinsi ya kumjulisha mwenzi wako unapotaka dakika chache kwako. Mwenzi wako atakupa nafasi ikiwa unahitaji
Kukubaliana juu ya masuala haya muhimu huleta utulivu, amani na umoja.

Ikiwa ndoa yako ina machafuko kwa sababu ya ukosefu wa utaratibu. Bado hujachelewa kufanya mazungumzo yatakayoleta makubaliano kuhusu masuala haya.

Add Comments


EmoticonEmoticon