Tuesday, April 29, 2025

Sanaa ya Kuongea na Mpenzi wako - Tazama Maujanja hapa

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


 SANAA YA KUONGEA NA MPENZI WAKO


1. Epuka kuzungumza naye kwa ukali. Usimfanye ajisikie kama unashindana naye

2. Akikosea Usimseme kwa ukali kufanya hivyo ni kuhatarisha penzi lako

3. Mpe nafasi na muda wa kuzungumza. Usitawale mazungumzo, muda wote

4. Kuwa mkweli. Usiwe mwanamke wa kumsema maneno makubwa na kutukana. Matusi yako yataghairisha mahusiano

5. Angalia sauti yako. Unaweza kuwa unasema jambo sahihi lakini sauti yako ikawa haipo sahihi. Wakati mwingine ujumbe wako haupokelewi vyema kwa sababu ya uwasilishaji wako

6. Usitoe mahaba ya kimya, hii huwa inamsukumo wa mbali

7. Usiwe mtu wa kutoa amri na maelekezo kama bosi wake kazini , atashindwa kukuvumilia.

8. Dumisha furaha katika mazungumzo yako, hali hii humfanya abaki katika mazungumzo yenu na mtaelewana

9. Zungumza naye mambo yanayochangamsha akili yake, yanayomfanya ajifunze; hali hii inamfanya afurahie kuzungumza nawewe. namaanisha Mazungumzo ya watu wazima

10. Kamwe usiwe na mazungumzo ya kumsifu mtu mwingine kitendo hiki kitamshushia hadhi hasa ukimzungmzia ex wako, baba yako, mchungaji wako, mtu mashuhuri au rafiki

Add Comments


EmoticonEmoticon