Tuesday, April 29, 2025

Mwanamke Mthamini Sana Mwanaume Wa Aina Hii

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


MWANAMKE MTHAMINI SANA MWANAUME WA AINA HII:


1. Mthamini mwanaume anayempenda mama yake mzazi hii inamaana. Amelelewa vizuri huko alikotoka

2. Mthamini mwanaume anayependa kusoma, maana atashinda kila aina ya mitihani. huyu ni mwenye hekima

3. Mthamini mwanaume mcheshi. Hutajuta kuishi nae maana hachoshi

4. Mthamini mtu anayewajari wageni na wasio wageni bila kujari huyu ni nani anacheo ganina huyu anaheshima. na moyo mwema

5. Mthamini mwanaume anayekupa muda wa kukusikiliza. utakuwa unaeleweka kila wakati kwake

6. Mthamini sana mwanamume ambaye wazo lake la kujifurahisha kwako linajenga. huyu anakuwa Amekomaa kiakili

7. Mthamini mwanamume anayewajibika kifamilia na yupo tayari juu ya kile unachotaka wewe. Muda wako hautapotea bure

8. Mthamini mtu anayemheshimu baba yake mzazi bila kujali jinsi baba yake alivyo. huyu Amejifunza uanaume wa kweli

9. Mthamini mwanaume ambaye hamtusi ex wake au ex wako hata kama mliachana kwa fujo. huyu Ni mtu anayeingia kwenye mapenzi kwa sababu sahihi

10. Mthamini mwanaume anayekuhitaji. hatakuacha njiani

11. Mthamini mwanaume anayeupa sababu ya kumpenda, anatunza siri juu ya kuona uchi na udhaifu wako. huyu Anakuamini

12. Mthamini mtu anayekubali kurekebishwa na kubadilisha mfumo wake akikukosea. Atakuwa mtu bora wa kukupenda

13. Mthamini mwanaume anayekuombea. Anajua wewe ni zawadi toha kutoka kwa Mungu

14. Mthamini mwanaume anayewaheshimu wanawake wengine. huyu Atakuheshimu zaidi

15. Mthamini mwanaume anayewapenda watoto wako huyu ni mfano wa baba bora. Mtu huyu atakuwa na urithi wa heshima

16. Mthamini mtu mwenye maono. Atakupa changamoto na kukujenga, huyu anajua anakokwenda

17. Mthamini mwanaume mwenye marafiki wazuri. Unaweza kuijua tabia ya mwanaume wako kupitia marafiki zake.

18. Mthamini mwanaume anayethamini urafiki kuliko penzi. huyu Atakuwa mwaminifu kwako

19. Mthamini mwanaume anayevutiwa na ndoto zako. huyu Anajali maisha yako ya baadaye

20. Mthamini mwanaume anayeheshimu maamuzi yako asiye kurupuka. huyu Anakuona kama mwenzi wa maisha yake

21. Mthamini mwanaume anayekusahihisha unapokosea na kukutia moyo na kukupa msukumo unapofanya jambo zuri. Anaona uwezo wako na hatapumzika hadi uwezo wako utimizwe. Mtu huyo ni mlinzi wa maisha yako

22. Mthamini mtu ambaye amekuwa thabiti kwenye mtazamo wake. huyu Unaweza kumtegemea

23. Mthamini mtu anayefanya kazi kwa bidii, anajituma na ana bidii hata akiwa na kidogo. Huyo mwanaume anaenda sehemu na siku moja atakufanya ujivunie

24. Mthamini mwanaume ambaye haopotoshwi na wanaume wengine wanapoona uzuri wako na kukutamani. huyu Ni mtu salama kwako

Add Comments


EmoticonEmoticon