Monday, April 28, 2025

Kuwa Mke mwenye Upendo na Bora kwa Mumeo - Fanya haya Mambo

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK

 

JINSI YA KUWA MKE MWENYE UPENDO NA BORA

1. Kumbuka kwamba mapenzi si jukumu la mume peke yake

2. Mpongeze mumeo akiwa amevaa vizuri na ananukia vizuri

3. Gusa paja la mumeo wakati anaendesha gari au ameketi karibu hasa unapotaka kumwambia jambo.

4. Wakati mwingine jaribu kutumia simu kumchombeza kwa maneno ya chumbani kiuchokozi

5. Chezea vidole vyake wakati nyinyi wawili mna mazungumzo ya kwenu binafsi na kujadiri maisha

6. Jaribu Kumbembeleza na kuweka kichwa chake kifuani mwako mkiwa wawili kitandani

7. Weka mkono wako kwenye mikono yake kama Malkia anayejua msimamo wake kwenye ndoa

8. Wakati mwingine vaa Mavazi yanayoweza kumsisimua mumeo hasa akiukuona umevaa katika chumba cha kulala

9. cheza nae ikiwa muziki basi cheza kwaajili yake na pia usisahau kumtania

10. Mwambie mambo yote ya chumbani unayoyapenda pamoja na mitindo unayoipenda ya mapenzi na ile unayotaka kumfanyia

11. jaribu kumsifia kwa ustadi wake akiwa kifuani kwako wakati wa mizagamuano na jinsi alivyofundi wa mapenzi anayofanya yanayokupa raha. Mwambie jinsi anavyokutia wazimu

12. Mtoe out kwa tarehe, usisubiri kila wakati apange yeye na sio kila siku mpate chakula nyumbani akti mwingine mnaenda kula nje

13. kumbusu, sio tu kwenye midomo bali pia kwenye mashavu yake, paji la uso wake, vidole vyake.

14. Jitolee kumtumikia kila saa uwe na tabasamu usoni na umtunze

15. Mwite majina maalum "Mfalme wangu", "Mpenzi", "Asali"

16. Jiamini na kuwa wewe mwenyewe, fanya mambo makubwa ukiwa mtu binafsi. Itamsisimua atajivunia kuwa na wewe

17. Mzungumzie sana hadharani, mtie moyo faraghani anapokuwa kwenye nyakati ngumu

18. Tafuta nafasi jinsi anayopenda akiwa kwenye michanganyo na umfanyie hivyohivyo mara kwa mara

19. Msaidie kuvaa na kuvua nguo zake, tai yake, koti lake na viatu

20. Wakusanye watoto na umsemee maneno mazuri kwa watoto katika kumthamini, mfanye ajisikie kuwa wa thamani akiwa nyumbani kwake bila kujali hali yake ya kifedha

21. Ukiwa na chochote Mnunulie zawadi anazozipenda

22. Andaa chakula anachopenda au muulize angependa kula nini

23. Mwambie unampenda. Wanaume wanapenda kuthibitishwa pia. Mwambie pia kile unachopenda kwake

24. Muulize siku yake imekuwaje? au ameshindaje kazini? Onyesha jinsi unavyomthamini na kumtunza

25. Fanya harakati za kuanzisha uchokozi mkiwa kitandani usisubir aanze yeye kila siku

26. Muombee dua kwa mungu abarikiwe. Wanawake wa maombi ni wa kimapenzi

27. Hudhuria mahitaji yake bila yeye kumuuliza kama vile kumtengenezea kikombe cha chai/kahawa anapofanya kazi.


Kwa sababu mmekaa pamoja kwa miaka mingi haimaanishi kwamba utaacha kumfanya ajisikie wa pekee. Ulimvutia na kumfanya ajione wa thamani na ndiyo maana akakufuata ili akupate, uendelee kuvutia na kumthamini ili uendelee naye; unapofanya hivyo, atatamani uwepo wako na kukupa kilicho bora zaidi. Mwanamke anayempenda mumewe, hujenga nyumba yake

Add Comments


EmoticonEmoticon