Monday, April 28, 2025

Fanya haya ili Umuone Mpenzi wako ni Mpya kila Siku - Hutamuona wa Kawaida kabisa

 Jiunge na Magroup yetu

TELEGRAM | FACEBOOK


Fanya haya ili Umuone Mpenzi wako ni Mpya kila Siku – Hutamchoka kabisa

 

Mwanamume na mwanamke wanapooana na kufanya ngono mara kwa mara, ni rahisi kujenga mazoea na kutengeneza njia ndogo za mapenzi na kufanya kila mtu kupunguza hamu kwa mwenzie na kumuona wa kawaida mpaka itokee siku mmoja kati yao awe na hamu ya tendo la ndoa. "Tayari mnapeana raha lakin za muda mfupi. 


Ifuatayo ndiyo njia halisi na halali na itakayokufaa ili usijenge mazoea na kumuona mkeo/mpenzi wako wakawaida

1. Kumkumbatia mwenzi wako. ni Kitu rahisi sana japo watu wengi huchukulia kawaida

2. Kumbusu mwenzi wako sehemu nyingi bila kuwekewa kizuizi na sehemu nyingine za karibu kama midomo, paji la uso, mashavu, vidole, mgongo, shingo nk kamwe usimuwekee mwenza wako vizuizi muache awe huru kwenye mwili wako muda wowote mkiwa wote.

3. Kubembelezana na mwenzi wako pamoja na kuvaa mavazi ya kustrii mwili wako kunaleta hamasa sana kwa mwanaume yeyote awe na hamu na wewe tafadhri usipende kujiachia au kukaa uchi na kuonyesha maungo yako kwa mumeo mwanaume akikuona mara nyingi ukiwa uchi huishiwa na hamu na kukfanya akuone wa kawaida.

4. Kushikana mikono na mwenzi wako hata kama kwa muda mfupi tu. ni kitu kizuri sana huleta hamasa na kuamsha hisia

5. Kuminya mkono wa mwenzi wako huonyesha kujali, na kumfanya ajioneu kama kwako ni mmoja, na mwenye upendo sana.

6. Jitahidi Kuusoma mwili wa mwenzi wako. Kuzingatia maeneo yake mengi ambayo akiguswa au kuchezewa humpa hamu mfano kama kwa babu/bibi, na chuchu hiyo itakusaidia.

7. Kumpongeza mwenzi wako akifanya jambo zuri zhumfanya ajione analindwa na kujaliwa

8. Kukaa uchi mara kadhaa kwa pamoja, sio kwa sababu mnataka kupeana michanganyo na minyongesho, bali ni kwa sababu mnataka kupeana raha na raha sio mpaka tendo la ndoa mnaweza mkacheza tu chumbani huku mkifurahishana.

9. Wakati mwingine kula kwa kutumia bakuli/sahani moja. ni jambo la muhimu chakula cha mumeo usiache aandae dada wa kazi

10. Kuangaliana, kuangalia movie pamoja na kubadirisha maeneo ya kupeana michanganyo hii pia huleta hamu

11. Kutenga muda wa kuwa wa kuwa pamoja na kutofautisha nyakati za kuwa kwenye mihangaiko ni mhimu sana.

12. kukaa chini na mwenzi wako Kuzungumzia kuhusu hisia zenu.
Ishara hizi unaweza kuona kama ndogo lakini zinaonyesha upendo kwa njia kubwa.

Inasikitisha jinsi mwanamume na mwanamke wanapochumbiana kwa furaha huku wakitarajia kuoana lakini wakioana mapenzi yanabadilika na kuanza kutopeana raha zinazostahili kwaajili ya kujenga mazoea 

Add Comments


EmoticonEmoticon